OSTAZ JUMA ATUPIA DONGO KWA WAPENDA MADEM WA KIZUNGU


Promota Ostaz Juma

Ostaz akipata Selfie katika eneo la Sanamu ya Kumbukumbu ya hayati Mahatma Gandhi ambaye baada ya kufa na kuchomwa moto, sehemu ya majivu yake inaelezwa yalikuja kumwagwa Mto Nile.
Ostaz akipata 'selfi' moja mbele ya lango la kuingilia mwanzo wa Mto Nile, uliyopo Jinja nchini Uganda ambako anadai amekwenda kutalii, kwani mbali ya kuwa ni sehemu ya kitalii, lakini pia ni sehemu ambayo imetajwa hata kwenye vitabu vya dini. Inaelezwa kuwa mto Nile ndiyo aliongamiziwa Firauni (Farao).
...ni muda wa ku chill na ku relax..
Mkewe, Bi Mariam akiwa na mwanae
...akijichana na samaki wa Mto Nile.......wasanii underground wanauliza mzee umekimbia Bongo na Mtanashati yake?
Promota Ostaz Juma (pichani), ametupia maneno kwenye akaunti yake ya Insta na facebook yanayoashiria kuwaponda ma brazamen wenye tabia ya kutoka na mademu wa kizungu, especially wenye umri mkubwa. Kwa mtizamo wake ameonesha tabia hiyo ni sawa na kujishushia heshima Watanzania kwani wazungu wanapokuja nchini huchukua dada zetu wenye mri mdogo.
"ndio maana kwa upande wangu mimi, penz langu la dhati nimeelekeza kwa mke wangu mpendwa Mariam Daudi Mchitinyi," sehemu ya maneno aliyotupia yalisema.
PICHA: Facebook/Instagram

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA