BINTI ALAZIMISHA KUFANYA MAPENZI NA WATOTO


Na Dustan Shekidele, Morogoro/Ijumaa
UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firahuni! Binti aliyefahamika kwa jina moja la Afsa (14), anayesoma darasa la 7, ametiwa nguvuni na jeshi la polisi akidaiwa kuwafanyia ukatili na kuwadhalilisha watoto wawili wa kiume (majina kapuni) wa mama yake mkubwa kwa kuwakang’ata nyeti zao akiwalazimisha kufanya nao mapenzi.
Binti anayefahamika kwa jina moja la Afsa (14) anayetuhumiwa kuwanyanyasa watoto wadogo.
Tukio hilo la kushangaza ambalo lilijaza umati wa watu , lilitokea wiki iliyopita katika mtaa wa Nyerere, Kata ya Mafisa, mkoani hapa.
Kamanda wa OFM, Mkoa wa Morogoro akiwa kazini, alipokea taarifa kutoka kwa wananchi wa mtaa huo wakimuomba afike fasta.
Bila kuchelewa kamanda alitia timu na kukutana na akina mama wawili ambao walishusha ‘vesi’ za tukio hilo:
Binti huyo akiwa chini ya ulinzi, wa pili kulia ni mmoja wa watoto walionyanyaswa na binti huyo.
“Sisi ni wakazi wa mtaa huu wa Nyerere ambao tunaishi na Mama Mese mwenye watoto wawili wa kiume, anaishi pia na mtoto wa mdogo wake (Afsa) aliyempa jukumu la kuwalea wanaye.
“Cha kushangaza Afsa amekuwa akiwafanyia ukaliti wa kutisha watoto hao. Leo amewatoboa macho na njiti ya viberiti kuwapiga mateke na kuwasukumiza ukutani, mbaya zaidi aliwang’ata nyeti zao alipokuwa akiwalazimisha kuduu nao.
Makamanda wa Polisi wakimchukua mtoto mwingine aliyenyanyaswa na binti mtuhumiwa.
“Kama majirani tumemuuliza mama Mese inakuwaje wanaye wanateswa kila siku na yeye hachukui hatua yoyote, akasema hataki kwenda polisi wala kwa mwenyekiti wa mtaa anaogopa mtoto wa mdogo wake atafungwa sasa sisi tumeamua kukuita uje kushudia tukio hili bichi,” walisema kina mama hao walioomba hifadhi ya majina.
Mwanahabari wetu alifika kwenye nyumba hiyo na kumkuta mama Mese akiwa na watoto wake hao wakiwa na makovu mwili mzima, alipoulizwa undani wa tukio hilo na kwa nini hatoi taarifa katika vyombo vya usalama? Alifunguka:
Binti anayetuhumiwa akichukuliwa kwenye pikipiki kwenda kituo cha Polisi.
“Mimi ni mfanyakazi pia mwanafunzi, nasoma chuo hivyo wanangu hulelewa na Afsa ambaye ni mtoto wa mdogo wangu. Kweli wanangu wamepigwa na kufanyiwa ukatili na huyu mtoto wa mdogo wangu lakini suala hili sitaki lifike popote, nimepanga kumrudisha kwao Moshi,” alisema Mama Mese.
Katika hali ya kushanga, paparazi wetu alipotaka kumhojia Afsa, mama huyo alikataa jambo lililowakera majirani na kuibua vurugu.
Baada ya vurugu kuwa kubwa, jirani mmoja aliwatonya polisi ambao walifika ndani ya muda mfupi na kufanikiwa kumkamata Afsa kumpeleka kituoni kwa ajili ya hatua za kisheria huku mjumbe wa serikali ya mtaa huo, Yusuf Juma akishuhudia tukio hilo na kulilaani.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA