CHELSEA,MANCITY NA TOTENHAM NJE YA F.A

Manchester City,Chelsea Southampton na Totenham zimeondolewa katika mechi za kombe la FA baada ya kuadhibiwa na timu kutoka daraja la chini la ligi ya EPL.
Timu hizo ambazo zinaongoza katika jedwali la ligi kuu ya Uingereza Zilishangazwa baada ya kushindwa nyumbani na wapinzani wao.
Hii ni mara ya pili kwa mabingwa wa ligi ya Uingereza Mancity kuondolewa nyumbani na Middlesborough ambao walishinda kwa 2-0.
Vilevile kilabu ya daraja la kwanza Bradford City ilionyesha mchezo wa hali ya juu ilipotoka nyuma 2-0 na kuweza kuwashinda viongozi wa ligi ya Uingereza Chelsea 4-2 katika mechi ya FA ilioijaa mbwembwe za aina aina.
Katika uwanja wa Totenham bao la Jeffrey Schlupp lilisaidia Leicester kuishinda Totenham.
Leicester ilikuwa nyuma kwa bao moja kabla ya kusawazisha na kuongeza la ushindi.
Uwanjani Southampton Mshambuliaji Marouane Chamakh alifunga mabao mawili na kuisaidia kilabu ya Crystal palace kupata ushindi wa 3-2 dhidi ya Southampton katika mechi iliokuwa na mchezo mzuri.
Matokeo ya FA
Cardiff 1 - 2 Reading FT
Chelsea 2 - 4 Bradford FT
Derby 2 - 0 Chesterfield FT
Man City 0 - 2 Middlesbrough FT
Preston 1 - 1 Sheff Utd FT
Southampton 2 - 3 Crystal Palace FT
Sunderland 0 - 0 Fulham FT
Tottenham 1 - 2 Leicester FT
                                                                                             CHANZO:BBC


Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA