PICHA: RUSHWA YA NGONO YAMNASA KANJIBAI

Stori:  richard Bukos na Issa Mnally/Ijumaa
Hii ni tuhuma nzito! Katika hali inayoonesha maadili Bongo yanagaragazwa kwa kiwango cha kutisha, mapema wiki hii jamaa mmoja mfanyabiashara mwenye asili ya Kihindi almaarufu Kanjibai au Ponjoro, alinaswa kitandani akiwa mtupu na mwanamke aitwaye Hidaya ambaye ni mke wa mtu, akidaiwa kudai rushwa ya ngono ili ampe ajira.
Kanjibai akiwa mpole baada ya kufumaniwa.
OFM YATONYWA
Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, ikiwa kwenye ‘mingo’ zake ilipewa ‘ubuyu’ na vyanzo vyake kwamba ifike katika nyumba moja iliyopo Tandale jijini Dar es Salaam kwani kulikuwa na zoezi la ufichuaji wa maovu.
MAOMBI YA KAZI
Kabla ya tukio hilo, ilidaiwa kwamba hivi karibuni Kanjibai na Hidaya walikutana maeneo ya Kariakoo jijini Dar ambapo mwanamke huyo alikwenda kutafuta kazi.
Ilidaiwa kuwa baada ya kusalimiana mazungumzo mengine yaliendelea huku jamaa huyo akitaka mambo matamu-matamu ya chumbani kwa ahadi ya ajira:
“Kazi kwishapata lakini lete ile kachori (rushwa ya ngono), mimi patia kazi wewe, sawasawa?”
...Akiomba kuachiwa baada ya fumaniza hilo.
KANJIBAI ATUMA VIMESEJI VITAMU
Ilidaiwa kwamba baada ya wawili hao kuagana, Kanjibai alianza kumchombeza Hidaya kwa ‘vijimeseji’ vitamu-vitamu kupitia mitandao ya simu za mkononi hasa hizi za kisasa za kuteleza ‘smart phones’.
Iliendelea kudaiwa kwamba siku ya siku, wakiwa nyumbani kwao maeneo hayo ya Tandale, Dar, mume wa Hidaya aligundua mchezo huo mchafu baada ya kunasa mawasiliano haramu kati ya Kanjibai na mkewe ambapo alianza kumbana ‘maiwaifu’ wake ampe ushirikiano wamshike ugoni.
UTETEZI
Ilidaiwa kwamba, katika utetezi wake, mwanamke huyo alimwambia mumewe kuwa jamaa huyo alikuwa akitaka mapenzi ili ampatie ajira kwenye kampuni moja iliyopo Kariakoo, Dar.
MTEGO WAANDALIWA
Baada ya kukubaliana, mume na mke waliandaa mtego ambapo Hidaya alimwelekeza Kanjibai anakoishi Tandale.Ilielezwa kwamba, Kanjibai, bila kujua kinachoendelea huku akiomba maelekezo katika kila hatua, alifanikiwa kufika kwa wanandoa hao na kuzama ndani.Ikasemekana kwamba, jamaa huyo alipotimba ndani alikaribishwa chumbani ambapo hakuchukua muda, akasaula nguo zote na kubaki mtupu akiwa tayari kutekeleza uzinzi.
BONGE LA FUMANIZI
Baada ya Hidaya kutoa ishara kwa mumewe kuwa mambo ‘yameiva’, OFM wakatonywa ambapo bila kuchelewa, kama kawaida yake, mkuu wa zamu aliwaagiza vijana wake ambao walitoka mkuku kwa kutumia pikipiki ziendazo kasi kuelekea eneo la tukio.
OFM ilipofika eneo la tukio ilikuta bonge la sekeseke la fumanizi likiendelea huku Kanjibai akiwa mtupu kitandani, chumbani kwa wanandoa hao akiomba msamaha kwa kutumia Kiswahili cha ‘makabachori’ huku akiahidi kutorudia mchezo huo mchafu.
KISWAHILI MBOVUMBOVU
“Iko samehe mimi bana, pana jua hii kama mke ya mtu, iko najua ishi peke yake, hapana ambiya mimi kama olewa, samehe mimi ngoja ita kaka yangu jua vizuri Kiswahili ongea na wewe lakini hapana peleka mimi polisi, iko ogopa sana pelekwa Segerea,” alisikika Kanjibai akijitetea huku akimuomba mume wa mwanamke huyo pamoja na ndugu zake wamsamehe na wasimpeleke polisi kwani anaogopa kupelekwa Gereza la Segerea jijini Dar.
MKONO WA SHERIA
Hadi OFM inaanua virago eneo la tukio, mume, mke na wapambe walikuwa katika taratibu za kufuata hatua zinazostahili ili kumfikisha Kanjibai kwenye mkono wa sheria.



ONYO
Gazeti hili linatoa onyo kwa vitendo viovu vya ngono na kushauri wote wanaohitaji wenza kufuata taratibu zinazostahili ili kupunguza kasi ya mafumanizi, maradhi na migogoro mbalimbali katika jamii la sivyo OFM ipo kazini kila sehemu, kila saa kuwaumbua. - Mhariri.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA