MBARONI KWA MAPENZI YA JINSIA MOJA

Makongoro Oging’ na Haruni Sanchawa/Uwazi
DUNIA imekwisha! Wasichana wawili warembo, Maua Sadick (24), mkazi wa Stakishari, Ukonga wilayani Ilala na Lucy Fred (23), mkazi wa Karakata jijini Dar es Salaam, wanashikiliwa katika Kituo cha Polisi Stakishari, Ukonga, Dar kwa kesi yenye jalada STK/RB/463/2015  wakidaiwa kufanya mapenzi ya jinsia moja.
Warembo, Maua Sadick (mwenye shati la draft) na Lucy Fred wakipozi kimahaba.
Warembo hao walikamatwa Januari 12, mwaka huu saa sita mchana, nyumbani kwa Maua wakidaiwa kufanya ngono kinyume cha sheria ya kujamiiana ambapo watu wa jinsia moja ni makosa kukutana kimwili.
NDUGU, MAJIRANI WAKERWA
Kwa mujibu wa habari za kipolisi, kukamatwa kwa Maua kulitokana na taarifa za baadhi ya ndugu na majirani zilizopelekwa polisi kwamba, wasichana hao wanapokuwa kwenye tendo la ndoa wamekuwa wakipiga kelele za udhalilishaji kwa familia zao.
Wasichana hao wakiwa maeneo tofauti.
WALISHAONYWA, HAWAKUSIKIA
Vyanzo makini kutoka jirani na makazi ya Maua vinadai kuwa, kutokana na hali hiyo, baadhi ya watu walijitolea kuwaonya wasichana hao kuwa na staha wawapo kwenye faragha yao lakini pia wao ni wanawake haiwezekani wacheze mchezo huo wenyewe kwa wenyewe lakini hawakutaka kusikia.
MAJIRANI WAFUNGULIA REDIO SAUTI YA JUU
“Ilifika mahali wakiingia chumbani kuanza mambo yao sisi majirani tunazidisha sauti za redio ili watoto wasisikie lakini na wao sauti zao zinakuwa juu kushinda za redio,” alisema jirani mmoja akiomba jina lake lifichwe ili kukwepa uhasama.
Alisema kutokana na hali hiyo waliamua kufikisha habari hizo polisi kwani ni kinyume cha sheria watu wa jinsia mmoja kukutana kimapenzi.
Mrembo Lucy Fred ambaye ni mpenzi wa Maua Sadick.
HISTORIA YA LUCY
Wakizidi kuzungumza na Uwazi, majirani hao walisema, Lucy ambaye ndiye anaitwa mke na Maua amekuwa akitoka nyumbani kwa wazazi wake Karakata kwa lengo la kumfuata Maua.
SIKU YA TUKIO
Ilisemekana kuwa, siku ya tukio, majirani walipoanza kusikia ‘zile sauti zao’, waliwapa polisi namba ya simu ya mtu wa jirani na Maua kwa lengo la kusaidia kufika nyumbani hapo.
“Polisi walipofika waligonga mlango kwa muda mrefu bila kufunguliwa na kelele za mahaba zilizidi kusikika.  Baadaye, nadhani wakati wanapumzika sasa, Maua alifungua mlango mkubwa na kukutana na macho ya polisi, wakambana na kumtaka waende wote alipo Lucy, wakaenda chumbani na kumkuta.
“Pia polisi walikuta kidude ambacho huwashwa kwa betri kilichodaiwa pia hutumika wakati wa tendo,” kilisema chanzo.
Warembo hao kama wanavyoonekana kwenye picha zao za instagram.
HISTORIA YA MAUA
Maua ni binti ambaye ni yatima, amekuwa akiishi mwenyewe kwenye nyumba hiyo kubwa ya familia  hivyo kumwita Lucy mara kwa mara kwa madai ya kufanya ufuska huo kwa vile wana uhuru.
Inasemekana kuwa, Maua siku zote amekuwa akivaa mavazi ya kiume licha ya kwamba, ni mwanamke kamili.
POLISI WASHANGAA
Taarifa kutoka vyanzo vya ndani ya jeshi la polisi zinadai kwamba, hata wakiwa mahabusu ya kituo hicho, wawili  hao wamekuwa wakioneshana mapenzi baina yao kitendo kilichowashangaza mahabusu wengine na polisi pia.
Uwazi lilifika nyumbani kwa Maua na kukutana na mdogo wake aitwaye Aziz ambaye alikiri kukamatwa kwa Maua na kwamba tangu akamatwe hajarudi na wala hajui kinachoendelea huku akisema asingependa kuzungumzia suala hilo kwa sababu ya kutupiwa lawama na wanandugu kwamba yeye ndiye aliyepeleka taarifa polisi.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Ilala, SACP Mary Nzuki.
“Mimi sikai hapa, nimefika hivi karibuni nikitokea mkoani. Ndugu wananituhumu mimi kuita polisi, sijui mtu aliyewapa askari namba yangu wakanipigia kama  wageni wanaokuja nyumbani, nikawapa ramani na walipofika ndipo nikagundua ni askari,” alisema Aziz.
Mwenyekiti wa  Serikali ya Mtaa, George Mtambalike alipohojiwa na gazeti hili ofisini kwake alithibitisha kukamatwa kwa wasichana hao kwa madai ya kufanya mapenzi ya jinsia moja na aliwatembelea Kituo cha Polisi cha Stakishari.



Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Ilala, SACP Mary Nzuki alikiri kukamatwa kwao na akasema uchunguzi unaendelea.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA