Mfanyakazi wa ndani matatani kwa tuhuma za kumbaka tajiri yake

RAIA wa Poland mwenye umri wa miaka 31 (jina linahifadhiwa), anadaiwa kubakwa na mfanyakazi wake wa ndani.

Tukio hilo limetokea alfajiri ya Septemba 14 katika kijiji cha Jambiaji Kibigija wilaya ya kusini Unguja, ambapo mtuhumiwa ni mfanyakazi wa jikoni.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, Juma Sadi Khamis, amethibitisha kutokea tukio hilo na kumtaja mtuhumiwa kuwa ni Kantenina Alois Jakob (34) mkaazi wa kijiji hicho.

Alisema kabla ya tukio hilo, mwanamke huyo aligombana na mume wake na kuamua kwenda kulala kwenye nyumba nyengine.

“Siku ya tukio mwanamke huyu aligombana na mume wake baada ya kurudi nyumbani wakitoka klabu ya starehe na kwenda kulala nyumba nyengine, huku mume akiendelea kulala kwenye yumba yao ya kawaida,” alisema.

Alisema mume alimjulisha mfanyakazi wao kuhusu tukio hilo, lakini ilipofika usiku mtuhumiwa alikwenda kwenye nyumba aliyolala bosi wake wa kike na kuingia ndani atakatekeleza kitendo hicho.

“Alikuta mlango uko wazi, akaingia ndani na akafanya kitendo hicho na kumsababishia maumivu makali na sasa mtuhumiwa anashikiliwa kwa upelelezi,” alisema.

Alisema mwanamke huyo alimefikishwa hospitali ya Makunduchi kwa matibabu na baadae kuhamishiwa hospitali kuu ya Mnazimmoja.

Daktari wa kitengo cha mkono kwa mkono hospitali kuu ya Mnazimmoja, Salum Omar Mbarouk, alikiri kumpokea mwanamke huyo na kusema alipomfanyia uchunguzi aligundua michubuko kwenye sehemu zake za siri na mikwaruzo ya kucha kwenye mapaja na kifuani.

Aidha alisema mtuhumiwa nae alifanyiwa uchunguzi kwa kupimwa HIV na baadae kukabidhiwa jeshi la polisi kuendelea na upelelezi.

Alitoa wito kwa wananchi wanaofanyiwa vitendo vya udhalilishaji kuwahi kufika kituoni hapo ili kupatiwa matibabu pamoja kutunza ushahidi utakaotumiwa wakati watuhumiwa wanapofikishwa mahakamani,

Madina Issa

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA