SERIKALI ITAHAKIKISHA VIFAA VINAPATIKANA

hewaaradar_a6036.png

Mahmoud Ahmad Arusha
Serekali imesema kuwa itaendelea kuhakikisha vifaa vya mamlaka ya hali ya hewa vinakuwa vya kisasa zaidi huku ikiwataka watanzania kufuata utabiri wa hali ya hewa kwani inawasaidia kujua hali ya hewa kwa faida yao ya kiamaendeleo.
Kauli hiyo imetolewa na naibu waziri wa uchukuzi dkt Chalres Tibeza wakati akifungua mkutano wa wakuu wa mashirika ya hali ya hewa wa nchi wanachama wa SADC unaofanyika jijini hapa huku akiwataka kuhakikisha viwango vya utabiri kwa nchi hizo vinakuwa ilikuendana na changamoto zilizopo.(Martha Magessa)

Tibeza alisema kuwa Taarifa za hali ya hewa ni muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi kwani zinasaidia kujua kesho itakuwa na hali gani ya hewa vile vile inamsaidia hata mkulima,mvuvi na wote kwani inasaidia kwenye maeneo mengi hata wasafiri wanaoenda kwenye biashara zao wakisafiri kwa kutumia ndege pia zinawasaidia hivyo ni wajibu kwa kila mwananchi kuzifuatilia na si kuzibeza.

Alisema kuwa kwa sasa utabiri wa hali ya hewa hapa nchini umefikia kiwango cha Asilimia 85% na wakahakikisha kuwa maeneo mengi yanakuwa na vifaa vya kuwawezesha kutoa utabiri kwa asilimia mia utakaosaidia kukua kwa sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa.

Nae Mkurugenzi wa miundombinu na huduma wa jumuiya hiyo(SADC) Remmy Makumbe alisema kuwa nchi hizo zinachangamoto kubwa ya kukabiliana nao ikiwemo uhaba wa vifaa utakaosaidia kukuwa kwa viwango vya kimataifa ya utabiri wa hali ya hewa,na kubadilishana uzoefo ikiwemo mbinu mpya za kukabiliana na chngamoto zinazozikabili nchi wananchama.

Alisema kuwa pamoja na changamoto mbali mbali zinazoikabili jumuiya hiyo ikiwemo michongo kutotolewa kwa wakati nan chi wanachama pia mkutano huo unajadili mapendekezo yatakao pelekwa kwa mawaziri wan chi hizo kupitia mapendekezo hayo.

Aidha kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa TMA hapa nchi Dkt.Agnes kijazi alisema kuwa kukuwa kwa setka hiyo ya utabiri wa hali ya hewa hapa nchini kunatokana na kuwa na vifaa vya kisasa vinavyosaidia utoaji wa utabiri wenye viwango na kuishauri serekali kusaidia upatikana wa vifaa zaidi kwenye sekta hiyo.

Dkt Kijazi alisema kuwa mkutano huo mkuu wan chi wanachama wa sekta ya hali ya hewa wa jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini SADC ni mkutano wa kuratibu mapendekezo yatakayo wasilishwa kwa mawaziri na baadae kwa wakuu wan chi wanachama.
Alisema kuwa Idara hiyo inasaidia sana kisayansi kujua hali ya hewa ikiwemo utunzaji wa mazigira ambayo yanasaidia kutobadilika kwa hali ya hewa ya eneo Fulani la nchi hivyo kuweza kuyaboresha mzingira yetu huku akiwataka wananchi kutunza mazingira kwa faida ya kutobadilika kwa hali ya hewa kwenye maeneo yao.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA