MEZ B NDANI YA SEKESEKE KUBWA LA UPIGAJI WA PICHA ZA UTUPU NA MAMISS

Na Mwandishi Wetu
Msanii wa kitambo wa Bongo Fleva aliyewahi kutamba na Kundi la Chamber Squad na ngoma yake ya taifa ya Kama Vipi, Moses Bushagama ‘Mez B’ anadaiwa kuwaaibisha ma-miss kwa kuwalazimisha kupiga nao picha wakiwa watupu.

Msanii wa kitambo wa Bongo Fleva wa Chamber Squad Moses Bushagama, ‘Mez B’ akijiachia na 'totoz' fukweni.

Tukio hilo la kidhalilishaji na lisilovumilika lilijiri juzikati kwenye Ufukwe wa Mikadi uliopo Kigamboni jijini Dar muda mfupi baada ya jamaa huyo ‘kushuti’ video ya ngoma yake mpya ya Shemeji.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, jamaa huyo aliwafuata warembo hao waliojitambulisha kwa majina ya Vicky na Rebecca waliokuwa kwenye swimming pool (bwawa la kuogelea) ambao ilisemekana kuwa siyo raia wa Bongo na huko wanakotokea ni ma-miss.

Ilidaiwa kwamba Mez B ndiye aliyewaomba kupiga nao picha lakini jamaa huyo ‘akaharibu’ baada ya kwenda mbele zaidi na kuanza kuwaminya ‘vifuu’ vyao kifuani vilivyoonekana ni vya saa sita vilivyokuwa wazi bila hata ‘braa’.
Mmoja wa ma-miss hao akiwa mtupu sehemu kubwa tu ya mwili wake.

Ilisemekana kwamba baada ya kupiga picha hizo, yeye (Mez B) aliwafowadia washikaji zake ndipo zikazagaa kupitia mtandao wa WhatsApp.

“Hawa wasanii wetu kweli ni majanga. Ona Mez B alichokifanya na hawa mabinti. Yaani wapo kama walivyozaliwa lakini yeye yupo freshi na nguo zake. Kama siyo kudhalilishana ni nini! Amewaaibisha sana. Lakini na wao hawakuona?” alihoji mrembo mmoja aliyefowadiwa  picha hizo na rafiki yake kwenye WhatsApp.

Baada ya kuzitia picha hizo kibindoni, gazeti hili lilimtafuta Mez B kisha kumbana kuhusu tukio hilo ambapo alijitetea kwa ufupi:“Wale ma-miss walikuwa wanaogelea vifua wazi kwa muda mrefu. Wao ndiyo walioniomba kupiga nao picha.”

Kumekuwa na kasumba ya kupiga picha za utupu kisha kuziachia mtandaoni kwa kudhani kuwa ni kujiongezea umaarufu lakini ukweli ni kujiondolea utu na heshima mbele ya jamii.

Chanzo:globalpublishers

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA