T.I KUFANYA MAKAMUZI YA FIESTA JIJINI DAR ES SALAAM, OKTOBA 18

RAPPA kutoka nchini Marekani, Clifford Joseph Harris,'T.I' ni mmoja wa wanamuziki watakaopiga shoo katika Usiku wa Fiesta 2014 ndani ya Viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.
T.I atafanya makamuzi pamoja na wakali wengine watakaokuwa kwenye listi ya kutoa burudani Oktoba 18, mwaka huu.

Staa huyo mwenye albamu nane ambazo ni I'm Serious, Trap Muzik, Urban Legend, King, T.I. vs. T.I.P., Paper Trail, No Mercy na Trouble Man: Heavy Is the Head ambapo nyingi kati yake zimefanya vizuri sana katika soko la muziki.
T.I ameshinda tuzo tatu za Grammy tangu aanze safari yake ya muziki. 

Baadhi ya singo kali alizoachia mkali huyo na kufanya vyema ni "Bring Em Out", "What You Know", "Big Shit Poppin' (Do It)", "Swagga Like Us" (FT Kanye West, Jay-Z na Lil Wayne), "Dead and Gone" (FT Justin Timberlake), "Ball" (FT Lil Wayne) na "No Mediocre" (FT Iggy Azalea).

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA