JIHADHARI, CHUPA YA MAJI NI HATARI


Ni kawaida sana siku hizi kupuuzia jumbe nyingi zinazotumwa kwenye makundi mbalimbali ya mawasiliano kwa sababu nyingi ya hizo huwa ni ngano tu. Ila mtu anapokuwa na muda anaweza kuulizia ukweli kutoka kwa wengine.

Ndicho nilichokifanya leo. Nilipuuzia ujumbe uliotumwa kwenye kundi moja (tizama picha hapo juu), nikidhani ni moja ya zile zinazotungwa ili kuwapa watu kiwewe tu, lakini baadaye nikapata wazo la kuutuma kwenye kundi jingine na kuuliza 'Inawezekanaje?" 

Majibu niliyopata yamenipa sababu ya kumshukuru aliyetuma ujumbe huo kwa kunisababisha niwe makini kuhusiana na hilo. Nimefahamishwa:

"Ni possible kabisa sis. Imeshatokea na ilimhusisha mtu namfahamu sema tu aligonga gari nyingine kwa nyuma. Chupa ya maji aliiweka kwenye ile nafasi kwenye gia pale kumbe aliposhika breki ikaanguka na hakujua so safari ikaendelea baadaye kidogo akashika breki kumbe imesogea kwenye pedal"

Mwingine pia akachangia:

"Subi hiyo ya chupa ya maji ilishanitokea mimi. Bahati nzuri nilikuwa napunguza spidi vs kusimama kabisa. I never thought chupa ya maji inaweza kusababisha."

Nimeona vyema nishirikishe na wengine hapa ili tujihadhari kabla ya ajali.

CHANZO: wavuti.com

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA