MABOMU YANAVYO PIGWA UBUNGO KUTOKANA NA VURUGU KUTOKANA NA MGOMO WA MADEREVA

https://igcdn-photos-b-a.akamaihd.net/hphotos-ak-xaf1/t51.2885-15/10956715_1569041313347185_1525563388_n.jpg 

Jeshi la Polisi limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya watu wanaoleta vurugu katika kituo cha mabasi Ubungo.

  Polisi Jijini Dar es Salaam wamelazimika kutumia mabomu ya machozi katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo kutuliza vurugu zinazofanywa na abiria pamoja na wananchi kufuatia mgomo wa madereva.

 Mgomo huo wa madereva wa mabasi na malori umeanza rasmi leo asubuhi nchi nzima na kuathiri kabisa sekta ya usafirishaji, ambapo Jijini Dar es Salaam mgomo huo pia umehusisha mabasi ya daladala.

Shuhuda wetu ameshuhudia katika neo la Ubungo bajaji na pikipiki nazo zinalazimishwa kugoma, Dereva akileta ubishi anapigwa na usafiri wake kuharibiwa.


 Mpaka sasa mabasi yanayotoka Mwanza kwenda mikoa mingine hayajaondoka kituo cha mabasi cha Nyegezi,madereva wote wamegoma baada ya serikali kuwapa miaka mitatu wawe wamekwenda shule ya udereva.

Kutoka Stendi ya Ibinzamata Shinyanga,pia hakuna gari inayoruhusiwa kutoka stendi 

 
Umati wa abiria wakiwa kwenye kituo cha daladala cha Darajani-Ubungo huku kukiwa hakuna daladala yoyote inayofanya kazi baada ya kutokea kwa mgomo wa madereva wa Daladala jijini Dar.
 
Baadhi ya abiria wakiwa wamepanda magari ya mizigo baada ya kukosekana kwa daladala maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam leo asubuhi. 
Mmoja wa abiria akiongea na dereva wa kibasi kidogo kuangalia kama kuna uwezekano wa kupata usafiri maeneo ya Mwenge jijini Dar.
Katika kituo cha mabasi cha Mpakani eneo la Mwenge zilionekana Bajaj zikipakia na kushusha abiria baada ya madereva kuingia kwenye mgomo leo asubuhi.


Habari  toka  Morogoro  zinaarifu  kuwa  Abiria wamejazana  katika  vituo  vya  daladala, bodaboda ndo zinatoa msaada  (kwa wale wenye uwezo).


Mdau   wa Malunde1 blog Kutoka  Kahama  anaarifu  kuwa  mpaka  sasa  hakuna  basi  hata  moja  lililotoka  kwenda  mikoani. 

Kutoka stendi ya Mwanza pia tunaambiwa hakuna hata basi moja imeruhusiwa kutoka

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA