Rais Kikwete amteua Mgaza kuwa Balozi Saudi Arabia

10 Apr 2
Hemed Iddi Mgaza
Hemed Iddi Mgaza

Rais Jakaya Kikwete amemteua Hemed Iddi Mgaza kuwa Balozi wa Tanzania Saudi Arabia.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK), Balozi Ombeni Sefue jana imesema uteuzi huo ulianza Machi 27.

Kabla ya uteuzi huo, Mgaza alikuwa Ofisa Mambo ya Nje Mkuu, Daraja la Pili na Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Mgaza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Abdillah Omar ambaye mkataba wake wa utumishi umekwisha.

via gazeti la Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA