STARS YAICHAPA 4-1 BENIN


Thomas Ulimwengu akikwaana na beki wa Benin (jezi nyeupe).

Kipa wa Benin, Farnoue Fabien akijaribu kuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na Nadir Haoroub 'Cannavaro' bila mafanikio. 

 Nadir Haoroub 'Cannavaro' (kushoto) akishangilia baada ya kuipatia Stars bao la kwanza. Kulia ni Oscar Joshua.(P.T)

Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick wakifuatilia mechi hiyo.

Amri Kiemba (wa pili kushoto) akipongezwa na wenzake baada ya kuifungia Stars bao la pili.

Mashabiki wa Stars wakifurahia ushindi.
KIKOSI cha Taifa Stars leo kimewapa raha mashabiki baada ya kuishushia kichapo cha mabao 4-1 timu ya Taifa ya Benin kwenye mechi ya kirafiki iliyochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Katika mechi hiyo, mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda.
Mabao mawili ya Stars yamefungwa kipindi cha kwanza na Nadir Haoroub 'Cannavaro' dakika ya 16 ya mchezo akiunganisha mpira kwa kichwa huku bao la pili likiwekwa kimiani na Amri Kiemba Ramadhan katika dakika ya 40. Mpaka mapumziko Stars walikuwa mbele kwa mabao 2-0. 
Thomas Ulimwengu aliiandikia Stars bao la tatu dakika ya 49 ya kipindi cha pili baada ya kupokoea krosi safi kutoka kwa Mrisho Ngasa. 
Juma Luizio aliifungia Stars bao la nne kwenye dakika ya 71 na kufanya matokeo kuwa 4-0 kabla ya Benin kupata bao lao la kufutia machozi kupitia kwa Suano Fadel dakika ya 92 ya mchezo. Mpaka mwisho wa mchezo, Stars 4-1 Benin.
(PICHA NA RICHARD BUKOS / GPL)

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA