AZAM TV YASAKA WAKALI WA UCHEKESHAJI, USAHILI KUFANYIKA UWANJA WA TAIFA DAR OKTOBA 10



Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizojaa vijana wengi wenye vipaji vikubwa katika mambo tofauti tofauti, lakini fursa ya kuonekana imekuwa adimu sana.
 
Ni kawaida kabisa kupita mitaani na kuwakuta vijana wenye uwezo wa kuchekesha na kuigiza, lakini hawana kwa kwenda.
Kwa kulitambua hilo kituo bora cha Azam TV kimedhamiria kutoa fursa kwa watu wote wanaojihisi wana vipaji vya uchekeshaji, lakini hawajapata nafasi ya kuonekana ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.
 
Katika kuhakikisa hilo, Azam TV imeandaa kipindi cha ucheshi cha Luninga kiitwacho WASAKATONGE COMEDY SHOW na usahili kwa ajili ya kutafuta wenye vipaji vya kuchekesha jukwaani na kuigiza vichekesho unatarajia kufanyika ijumaa ya Oktoba 10, 2014, kuanzia saa 2:00 asubuhi mpaka saa 12:00 jioni ndani ya uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
 
Usahili huo utajali misingi ya haki na mwenye uwezo pekee ndiye atakayepata nafasi ya kusonga mbele, hivyo kila mtu afike kujaribu bahati yake.
 
Mchakato huu utaegemea zaidi katika kigezo cha Ubunifu kwa minajili ya kuchekesha, kuwa mwepesi katika ucheshi, kuwa na mawazo ya haraka katika ucheshi na jinsi gani anaweza kushirikiana na wenzako kama timu moja.
 
Kwa mshiriki yeyote yule kutoka nje ya mkoa wa Dar es salaam bado ana nafasi ya kushiriki usahili isipokuwa gharama zote zitakuwa juu yake.
Ili kutengeneza timu ya WASAKATONGE mchakato utakuwa wa awamu mbili;-
 Mosi; kutakuwa na usahili wa wazi utakaofanyika uwanja wa ndani wa taifa (Indoor); kwa wale wachache watakaopita kulingana na hitaji la kamati watapewa utaratibu juu ya kipi kitakachoendelea kwa mzunguko wa pili.
 
Pili; kutakuwa na mchujo utakaopelekea kuchaguliwa kwa watu wachache, wasiozidi kumi na hao ndio watakaotengenezwa kwa kupatiwa mafunzo ili kuwa wachekeshaji/waigizaji. Watakaobahatika watakuwa  WASAKATONGE wa Azam tv.
Mambo ya Zingatia!!!
Usaili huu ni wa wazi, Wasahiliwa watapaswa kujigharamia usafiri na chakula, Hakuna zawadi kwa washindi. Mafunzo ya uchekeshaji yatatolewa kwa washindi 10

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA