MREMBO AMCHOMA VISU MBONGO SAUZI

 
Stori: Mayasa Mariwata na Shani ramadhani
WIVU
wa mapenzi bwana! Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la David Patrick Chagu (pichani) aliyekuwa akiishi Jimbo la George nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’  amekumbwa na mauti kwa kuchomwa visu na mpenziwe aliyefahamika kwa jina moja la Monica.
Waombolezaji na mama wa marehemu, Rose Ndunguru (wa pili kulia) wakiwa katika hali ya simanzi.
Tukio hilo lilitokea Oktoba 2, mwaka huu na marehemu alizikwa Oktoba 14, mwaka huu katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar huku akiwa ameacha mtoto wa miezi nane.
Marafiki wa karibu wakimuaga mpendwa wao marehemu David Patrick Chagu.
Kwa mujibu wa chanzo, marehemu alichomwa visu na mpenzi wake huyo ambaye ni Mzungu kwa madai ya wivu kufuatia kutomwona kwa siku tatu na kumhisi ana mpenzi mwingine.
Waombolezaji wengine wakiomboleza katika msiba huo wakati wa mazishi.
Akizungumza na Uwazi kwa majonzi makubwa, mama mzazi wa marehemu, Rose Ndunguru ambaye ni Katibu wa Umoja wa Wanawake wa CCM Kata ya Ubungo alisema alipatwa na simanzi kubwa kutokana na kitendo hicho alichokifanya mkwewe ambaye alikuwa akimpenda mno na kutoamini alichomtendea mwanaye.
Padri akiuombea mwili wa marehemu David Patrick Chagu.
“Naumia sana jamani sijui nielezeje! Chanzo cha yote Monica alinipigia simu akasema ana siku tatu hajaonana na David kwa kuwa walikuwa hawaishi wote.“Alisema nimpigie simu David, nimwambie mtoto anaumwa, ndipo mwanangu akaenda na kumkuta mtoto mzima isipokuwa alikuwa akisumbuliwa na mafua.”
Mwili wa marehemu David Patrick Chagu ukishushwa kaburini.
“Siku iliyofuata, kwa kuwa David ni mfanyabiashara mbali ya kuwa ni mwanafunzi katika Chuo cha Wescaptown, akiwa anatoka kwenye biashara zake alikwenda nyumbani kwa Monica kumrudisha shemeji yake wa kiume akiwa na gari.
Waombolezaji wakiweka mashada ya maua kwenye kaburi la David Patrick Chagu.
“Aliposhuka tu akiwa eneo la wazi la barabara ndipo Monica akamchoma visu vitatu, kifuani na cha mkononi bila huruma,”alisema mama huyo.Aliongeza kuwa, kutokana na  tukio hilo ambalo lilitokea usiku wa Alhamisi mwanaye alikimbizwa kwenye Hospitali ya Mozaribay iliyopo palepale George, lakini baada ya nusu saa akafariki dunia.
David Patrick Chagu enzi za uhai wake.
“Monica alikamatwa asubuhi yake na kuwekwa ndani japo mpaka sasa yupo nje kwa dhamana.
“Inasikitisha sana kwani sasa amekuwa akinisumbua kwenye simu akitaka matumizi ya mtoto na kuniambia nimsamehe kwa alichofanya kwani hakukusudia.”Mama huyo alisema yeye ameshamsamehe Monica kwa yote yaliyotokea na kumwachia Mungu.


chanzo:global publishers

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA