CHADEMA, CUF, NCCR MAGEUZI NA NLD VYATILIANA SAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO


Viongozi wa juu wa vyama vinne vya siasa nchini Tanzania vimeingia makubaliano ya ushirikiano wa shughuli mbalimbali za siasa hii leo na miongoni mwa mambo hayo ni kusimamisha wagombea wa pamoja katika uchaguzi wa Serikali za Mtaa na Uchaguzi Mkuu wa wabunge, madiwani, wawakilishi na Rais 2015. Kutoka kushoto ni James Mbatia wa NCCR-MAGEUZI, Prof Ibrahim Li[pumba wa chama cha Wananchi CUF, Freeman Mbowe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Dk. Emmanuel makaidi wa NLD wakionesha hati yao ya makubaliano waliyoisaini jana katika viwanja vya Jangwani Dar es Salaam 

Viongozi hao wakishangilia kuzaliwa kwa ushirikiano huo huku makatibu wao wakiwa wameketi. kwa kuangalia siani za makubaliano wa ushirikiano bofya soma zaidi. 

Wafuasi, wanachama, wa vyama vya siasa vinavyounda ukawa wakifuatilia mkutano huo ambao ulianza kwa kuimba wimbo wa Taifa huku wanachama hao wakiwa wamekaa jambo ambalo lilielezwa na viongozi wao kuwa uzalendo ni ndani ya moyo. Chini ndio mambo waliyokubaliana.



Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA