KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA ASISITIZA KUWA ISRAEL NI UTAWALA WA KIBAGUZI



Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa asisitiza kuwa Israel ni utawala wa kibaguzi

Kwa kuzingatia kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel unatambuliwa kuwa moja ya nembo za ubaguzi katika uga wa kimataifa, ukweli ni kuwa hata viongozi wa Umoja wa Mataifa pia wamekiri kuhusiana na suala hilo kutokana na miamala ya kibaguzi inayotekelezwa na utawala huo.

Katika uwanja huo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa Israel inatekeleza siasa za kuangamiza kizazi huko Quds inayokaliwa kwa mabavu.
Ban Ki-moon amesema katika ujumbe wake uliosomwa jana na mjumbe wake kwenye "Mkutano wa Kimataifa wa Quds" huko Jakarta mji mkuu wa Indonesia kwamba sababu inayowatia hasira Wapalestina katika ardhi za zinazokaliwa kwa mabavu ni ukaliaji mabavu wa Israel pekee.

Ujumbe huo umebainisha kuwa, mwaka 1967 Israel ililiunganisha eneo la Baitul Muqaddas ya Mashariki na maeneo mengine iliyoyaghusubu na sasa inajaribu kuendeleza siasa zake hizo ili kuyaweka chini ya udhibiti wake maeneo mengine zaidi ya Baitul Muqaddas na kupunguza idadi ya wakazi wa Kipalestina katika maeneo hayo.

Ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa vilevile umesisitiza kuwa Israel inatekeleza siasa za kuangamiza kizazi huko Baitul Muqaddas; huku ikiwafukuza raia wa Kipalestina majumbani mwao. Ban Ki-moon kwa mara nyingine tena amesisitiza kuwa kwa mtazamo wa Umoja wa Mataifa ni kuwa ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi unaofanywa na Israel ni kinyume cha sheria na unakinzana na sheria za kimataifa.
Hakuna shaka kuwa ubaguzi wa hali ya juu wa utawala wa Kizayuni unadhihirisha ni kwa kiwango gani jamii ya kimataifa inavyokabiliwa na utawala ambao ni mbaya zaidi kuliko utawala wa ubaguzi wa rangi wa Apartheid na ufashisti.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa radiamali yake kwa vitendo vya ukandamizaji na kidhulma vya utawala wa Kizayuni wa Israel katika hali ambayo utawala huo unaendelea kushadidisha miamala yake mibovu na misimamo ya uhasama na kibaguzi dhidi ya Wapalestina; jambo linaloitia wasiwasi jamii ya kimataifa.

Kuongezeka jinai na kuuawa kila uchao raia wa Palestina wasio na hatia khususan katika wiki za hivi karibuni ambapo hadi sasa Wapalestina 125 wameuawa shahidi na wanajeshi wa Israel, kunatokana na utawala huo kuwa na mizizi na asili ya mitazamo ya kibaguzi.

Siasa za kibaguzi na maangamizi ya kizazi yanayofanywa na utawala wa Kizayuni yanadhihirisha namna utawala huo unavyojishughulisha zaidi na kutenda jinai na kukiuka haki za mataifa na kaumu mbalimbali, kama ilivyokuwa katika zama za Wanazi huko Ujerumani, Mafashisti huko Italia, na mfumo wa ubaguzi wa rangi yaani (Apartheid) nchini Afrika Kusini.

Miamala isiyo ya kibinadamu inayotekelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel imeitia wasiwasi jamii ya kimataifa na itakumbukwa kuwa mwaka 1975 Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa pia lilitoa azimio nambari 3379 na kuutaja utawala wa Kizayuni kuwa ni sawa na utawala wa kibaguzi, kufuatia malalamiko ya jamii ya kimataifa dhidi ya utawala huo ghasibu.

Japokuwa azimio hilo lilifutwa kati kati ya muongo wa 90 kufuatia mashinikizo ya serikali za Magharibi na baada ya kuathiriwa na madai ya uwongo ya utawala wa Kizayuni kwamba inataka amani, lakini utendaji wa utawala wa Kizayuni umeonyesha utawala huo haujapunguza hata chembe siasa zake hizo za kibaguzi bali umezishadisisha; na huu ni uhakika wa mambo ambao ameukiri wazi Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Israel.

Hii ni katika hali ambayo kamati ya kupambana na ubaguzi ya Umoja wa Mataifa pia hivi karibuni ilibainisha wasiwasi wake kuhusu hatua ya Israel ya kupuuza sheria za kimataifa na kutoheshimu haki za binadamu na kutahadharisha kuhusu hali mbaya waliyonayo raia wa Kipalestina katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu. Kamati hiyo imesisitiza kuwa utawala wa Kizayuni unapasa kusailiwa.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA