Taka zilizokusanywa Desemba 9 zizolewe kabla ya Desemba 20


Waziri George Simbachawene akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo mjini Dodoma

WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora, George Simbachawene amewaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurungenzi wote wa halmashari nchini kuhakikisha wanazoa taka zote zilizokusanywa wakati wa siku ya uhuru kabla ya tarehe 20 mwezi huu.

Kauli hiyo aliitoa wakati alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati wa kikao cha kumkaribisha katika ofisi ya TAMISEMI mjini Dodoma.

Alisema kuwa hataki kuona hadi ifikapo tarehe 20 ya mwezi huu kuwa uchafu unaendelea kulalamikiwa:
“Hadi ifikapo tarehe hiyo sitaki kusikia uchafu bado haujaondolewa katika maeneo ulipokusanywa toka Siku ya Uhuru, lakini pia unapoondolewa huo kuna uchafu mwingine unakuja hivyo basi watendaji wanaohusika wahakikishe kuwa wanaanda maeneo ya kuupeleka,”alisema Simbachawene.

Naibu Waziri wa wizara hiyo Suleiman Jaffo, aliwataka watumishi wa TAMISEMI kubadilika katika utendaji wao wa zamani ili waweze kuongeza ukusanyaji wa mapato na kuweza kuboresha maisha ya wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA