HOSPITALI YA MUSOMA YAKABILIWA NA TATIZO LA UPUNGUFU WA DAMU
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
HOSPITALI ya mkoa wa Mara mjini Musoma bado inakabiliwa na tatizo kubwa
la upungufu wa damu jambo ambalo limetajwa wakati mwingine kuchangia
vifo hasa vya wanawake wajawazito na watoto.
Mganga mfawidhi wa
hospitali ya mkoa wa Mara Dk Joseph Nyamagwira Amesema kupungua kwa
damu katika hospitali hiyo kumetokana na mwamko mdogo wa wananchi katika
kuchangia damu hiyo hivi sasa.
Amesema ingawa hospitali imekuwa ikijitahidi kuhifadhi sehemu ya damu
kwa ajili kukabiliana na dharura,lakini wakati mwingine benki ya damu ya hospitali hiyo imekuwa ikiishiwa kabisa ikiwemo damu ya kundi la O
jambo ambalo limekuwa likisabisha wagonjwa wa kundi hilo kupoteza
maisha.
Hata hivyo Dk Nyamagwira,amesema pamoja na ndugu za
wagonjwa kujitolewa kuchangia damu hiyo,lakini kutokana na magonjwa
yaliopo hivi sasa damu hiyo imekuwa haitumiki kumuongezea mgonjwa wakati
huo hadi ipelekwe kwenye vipimo vikubwa katika hospitali ya rufaa ya
Bugando jijini Mwanza ambapo zaidi ya asilimia 50 ya damu hiyo mara
nyingi imekuwa ikimwagwa baada ya kubainika kuwa si salama.
Kwa
sababu hiyo ametoa wito kwa taasisi za shule,vyuo,majeshi na watu
binafsi kurudia zoezi kama ilivyokuwa awali kwa kujitolea kutoa damu
ambayo itasadia kuokoa maisha ya watu wengine wakiwemo watoto,wanawake
wajawazito na wananchi wanaopatwa na majanga ya ajali.
Taarifa hii ni kwa hisani ya Agustino mgendi mwakilishi wa blog hii kutoka Musoma.
Zao la pareto ni miongoni mwa mazao ambayo wakulima wamekuwa wakipunguza na kuacha kuyalima kabisa, huenda ni kutokana na bei yake kuwa chini au soko sumbufu. Kamera ya Benjamin Kaminyonge ilipita maeneo ya wilaya ya Makete, kata ya Matamba na kuona zao hilo likiwa kwenye shamba la ekari moja ndani ya kijiji kizima huku kukiwa na mazao kama mahindi, ngano, maharage na alzeti kwa wingi. (picha: benjaminkaminyoge.blogspot.com)
pande hizi ni za kariakoo maeneo ya msimbazi nilikuwepo mida ya mchana,pande hizi watu hawakosekani kuna nyomi ya watu kama unabisha nenda saa nane usiku kariakoo na utakuta watu wanapiga mzigo kama kawaida!!!!
Comments
Post a Comment