SIMBA YAPAA ALGERIA NA MATUMAINI KIBAO



Wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya Afrika, Simba SC wameondoka alfajiri ya leo Dar es Salaam kuelekea Algeria kwa ajili ya mechi ya marudiano, Raundi ya Pili Kombe la Shirikisho la Soka Afrika dhidi ya wenyeji ES Setif, wakipitia Algeria.
Simba imeondoka ikisema ina matumaini makubwa ya kuitoa ES Setif katika mchezo huo utakaofanyika Ijumaa wiki hii.
Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema wachezaji wapo katika ari nzuri na kwamba wimbo wao ni ushindi. Kamwaga aliwataja viongozi watakaofuatana na timu hiyo kuwa ni Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo Damian Manembe na Kamwaga.
Alisema benchi la ufundi watakaokuwepo ni Kocha Mkuu Milovan Cirkovic, Kocha Msaidizi Amatre Richard, kocha wa makipa James Kisaka, daktari wa timu Cosmas Kapinga, Nyagawa na mtunza vifaa Kessy Rajab.
Aliwataja wachezaji waliopo kwenye msafara ni Juma Kaseja, Ally Mustafa, Nassor Masoud, Shomari Kapombe, Amir Maftaha, Juma Nyoso, Kelvin Yondani, Victor Costa, Obadia Mungusa, Jonas Mkude, Patrick Mafisango, Mwinyi Kazimoto, Haruna Moshi, Salum Machaku, Uhuru Suleiman, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi, Edward Christopher, Derick Walulya na Gervais Kago.
Naye Kocha Mkuu, Milovan alisema wamejipanga vilivyo na kwamba wataufanyia kazi udhaifu uliojitokezakwenye mchezo wa kwanza na kuwaomba mashabiki wasiwe na wasiwasi na kuwa watarejea na ushindi.
Simba ilishinda mchezo wa kwanza wiki moja iliyopita mabao 2-0, hivyo sare ya aina yoyote au isipofungwa zaidi ya bao 1-0 itakuwa imesonga mbele.
Katika mchezo huo, Simba baada ya ushindi wa awali wa 2-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, inahitaji hata sare au kufungwa si zaidi ya 1-0 ili kusonga mbele. 

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA