UTAPELI MPYA KATIKA FOLENI ZA MAGARI WAZIDI KUSHIKA KASI JIJINI DAR

Kuna aina mpya imeingia siku hizi jijini Dar es Salaam.

Unapokua katika yale  maeneo ya foleni kali muda ya kwenda kazini  ama kurudi nyumbani, anatokea mtu kwa mbele kama anavuka na kukuonyesha ishara yaani kama fungua vioo, na kisha anakupa ishara zaidi kua uangalie nyuma ya gari yako (wakati huo wewe upo kwenye foleni na hivyo unazingatia magari yanasogee ili na wewe usogee), wakati yule mtu wa mbele yako yupo "busy" kukupa ishara mbalimbali, kumbe ile ni kukuvuruga akili. Papohapo utasikia   kitu  kama kishindo kwa nyuma ya gari lako (ni mtu kajigongesha kwenye gari yako na kujiangusha ili wadai umemgonga) kumbe ni mwenzie yule wa mbele aliyekuwa anakupa ishara za uongo na kweli. Wote ni matapeli.

Kitendo hiki kinafanyika haraka sana, yaani kufumba nakufumbua, yule mtu anapojigongesha tu kwenye gari, wenzake watatokeza pasipojulikana na kulizunguka gari.

Utakapofanya uungwana wa kufungua vioo vyako au kushuka toka kwenye gari lako, ndipo kosa unapokuwa umelitenda kwani unawaachia mwanya wa wao kukuliza kwani kwa "speed" ya ajabu mwenye kuchukua simu, pochi ama briefcase yako au chochote cha thamani kilicho katika gari lako, watafanya hivyo "fasta" sana. Watakuwa wanakuzunguka na kusema ''umeua, umeuaa....''  ili kukutia hofu, na wewe utastuka na kumjali yule jamaa alieanguka pale chini. Baada ya dakika chache tu, unajikuta umebaki wewe na wengine wote wamekimbia, salama yako wasikupige kwani wakati mwingine wanadiriki kukupiga ili kukuogofya na ujitetee.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA