KITIVO CHA ELIMU UDOM CHAIBUKA NA USHINDI WA VIKAPU 58 KWA 53 DHIDI YA DODOMA SPURS KATIKA LIGI YA MPIRA WA KIKAPU MKOANI DODOMA

Mchezaji wa Timu ya Mkoa alipoipatia timu goli katika ligi ya mpira wa kikapu iliyoanza leo katika viwanja vya kitivo cha sayansi ya Jamii, Sanaa na Lugha cha Chuo Kikuu Cha Dodoma
Kashikashi ikiendelea hapo huku wengine wakitaka kushinda huku wengine wakitaka kuokoa goli lisiingie
Mchezaji wa Timu ya Kikapu ya Dodoma Spurs (Timu ya Mkoa) akijaribu kumpita Mchezaji wa timu ya kikapu ya kitivo cha elimu cha chuo kikuu cha Dodoma katika mchezo wa ligi ya mpira wa kikapu iliyoanza leo na timu ya Kitivo cha Elimu cha Chuo Kikuu Cha Dodoma Chaibuka Mshindi Kwa Vikapu 58 kwa 53 Dhidi ya Timu ya Mkoa (DODOMA SPURS)
Baadhi ya Wanafunzi na Wadau wengine wakifuatilia mchezo huo uliokuwa ukichezwa kati ya Timu ya Mpira ya Kikapu kutoka Kitivo Cha Elimu Cha Chuo Kikuu Cha Dodoma Na Timu ya Dodoma Spurs (Timu ya Mkoa) ambapo timu ya kitivo cha elimu cha Chuo Kikuu Cha Dodoma iliibuka na ushindi wa Vikapu 58 kwa 53 dhidi ya Timu ya Mkoa Wa Dodoma (DODOMA SPURS) katika ligi ya mpira wa kikapu inayoendelea kufanyika katika viwanja vya Kitivo Cha Sayansi ya Jamii,Sanaa na Lugha cha Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM).
Mchezaji wa timu ya Kitivo cha elimu cha Chuo Kikuu Cha Dodoma akijaribu kufunga katika mechi ya ligi ya mpira wa kikapu iliyoanza leo na timu hiyo ya walimu kuibuka washindi kwa vikapu 58 kwa 53 dhidi ya Timu ya Kikapu Ya Mkoa Wa Dodoma
Mpira ukiingia kwenye nyavu na kupelekea timu ya kitivo cha elimu cha Chuo Kikuu Cha Dodoma kushinda
Mpira ukielekea nyavuni hapo

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA