AFISA WA NEC ASEMA WANAVYUO WAJIANDIKISHE BILA HOFU YA WAPI WATAKUWA SIKU YA UCHAGUZI

03 Mar20
Washiriki kutoka vyuo mbali mbali vya Mkoa wa Mbeya.

Wasomi wa Vyuo vikuu Mkoa wa Mbeya wamesema ratiba ya uchaguzi si rafiki kwa wanafunzi na kuwa inawapa mashaka ikiwa wataweza kushiriki kwenye kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Wakizungumza na kwenye mdahalo wa vyuo vikuu uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Chuo kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU) ulioandaliwa na Chama cha Walimu wanaofundisha masomo ya Siasa (CETA), walisema masharti yaliyowekwa na tume ya uchaguzi kwamba ni lazima kila mtu apige kura katika eneo alilojiandikishia linawabagua wanafunzi kutokana na muda wa uchaguzi kuwa eneo tofauti na alipojiandikishia. Walisema asilimia kubwa ya wanafunzi hujiandikisha aidha akiwa chuoni ama nyumbani lakini siku ya uchaguzi huenda akawa sehemu tofauti na alipojiandikishia jambo ambalo linamnyima haki yake ya kupiga kura na kuchagua viongozi.

Wanafunzi hao walishauri kuwa endapo tume itaendelea kusimamia msimamo wake ni bora wanafunzi wakawekewa utaratibu wa kumchagua Rais kwa kuwa ni kiongozi wa Kitaifa tofauti na Wabunge na Madiwani ambao wanapaswa kuchaguliwa na wakazi wa eneo husika.

Afisa Elimu ya mpiga kura na elimu kwa umma kutoka tume ya uchaguzi, Salvatory Alute alisema ni vema vijana wakajitokeza kujiandikisha kwenye daftari la kudumu bila kuhofia ni wapi watakapokuwepo siku ya uchaguzi.

Alisema zoezi la kujiandikisha ni muhimu kutokana na kutolewa vitambulisho vipya tofauti na ambavyo tayari vipo kwa walioandikishwa zamani na kushiriki chaguzi zilizopita.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA