TAARIFA YA KINYANG'ANYIRO CHA KUMPATA MSHINDI WA TUZO YA JAMII

Taarifa ya kinyang'anyiro cha kumpata mshindi wa tuzo ya jamii



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU TUZO YA JAMII  ITAKAYOTOLEWA TAREHE 13 APRIL 2015 KATIKA UKUMBI WA JULIUS NYERERE INTERNATIONAL CONVENTION CENTRE, JIJINI DAR ES SALAAM

 

 
MGENI RASMI: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dokta Jakaya Mrisho Kikwete
 

 
WAGENI WAALIKWA
Mara baada ya Hafla ya Tuzo ya Jamii ambapo Washindi wote watapewa Tuzo na Mgeni Rasmi, Kutakuwa na Dhifa ya Kitaifa ya Tuzo ya Jamii ambayo itahudhuriwa na wageni wafuatao:
 

 
  • Wapewa Tuzo,
  • Familia za wapewa Tuzo,
  • Viongozi Waandamizi wa Serikali,
  • Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania,
  • Viongozi wa vyama vya siasa na kijamii na Wafanyabiashara,
  • Taasisi zisizo za kiserikali,
  • Watu Mashuhuri na
  • Wawakilishi kutoka makundi yenye mahitaji maalum ambapo kwa mwaka huu watawakilishwa na Watu wenye Ulemavu wa Ngozi-Albino
 

 
MUHIMU:
 
Tanzania Awards International Ltd imepanga kufanya hafla ya utoaji wa Tuzo ya Jamii na kisha Dhifa ya Kitaifa ya Tuzo ya Jamii siku ya tarehe 13 ya mwezi April ya kila mwaka kwa malengo ya kuadhimisha Kumbumbuku ya siku ya kuzaliwa  Baba wa Taifa,  Hayati Mwalimu Julius Kambarege Nyerere.
 

 
Kuhusu Tanzania Awards International Limited
 
Tanzania Awards International Limited ni kampuni iliyosajiliwa kisheria nchini Tanzania kwa Malengo ya Kufanya tafiti mbalimbali, Kutoa ushauri wa kisheria na kijamii, kuandaa na kuratibu matukio pamoja na Uandaaji na Utoaji wa Tuzo Ya Jamii.
 

 
Maana ya Tuzo ya Jamii
 
Tuzo ya Jamii ni Tuzo inayotolewa kwa Taasisi na Watu binafsi kutokana na Mchango na Jitihada zao katika kusaidia na kutetea maslahi ya Jamii.
 

 
Malengo ya Tuzo ya Jamii
 
  • Kutambua, Kuthamini, Kuunga Mkono na Kutoa Tuzo kwa Taasisi au Mtu Binafsi kutokana na Mchango na Jitihada zake katika kusaidia na kutetea maslahi ya Jamii.
 
  • Kuikumbusha Jamii kuona umuhimu, kujali na Kuunga Mkono jitihada zinazofanywa na Taasisi au Mtu Binafsi katika kuleta Ustawi na Maendeleo ya Jamii
 

 
VIPENGELE VYA TUZO YA JAMII 2015
 
Vipengele vya Tuzo ya Jamii, hubadilika kila mwaka kulingana na aina na matokeo ya Utafiti unaofanywa na Tanzania Awards International Limited. Kwa mwaka huu (2015), Tuzo ya Jamii itakuwa na Vipengele Vikuu vinne (4) vifuatavyo:
 

 
  1. Tuzo ya Jamii 2015
  2. Tuzo ya jamii –Tuzo ya Heshima
  3. Tuzo ya Jamii ya Haki za Binadamu
  4. Tuzo ya Jamii kwa Mwanasiasa mwenye mafanikio katika siasa za Tanzania
 

 
UFAFANUZI WA KILA KIPENGELE CHA TUZO YA JAMII 2015
 

 
  1. Tuzo ya Jamii 2015
 
Tuzo hii itatolewa kwa Taasisi au Mtu Binafsi kutokana na mchango na jitihada zake katika kusaidia na kutetea Jamii.
 

 
Mshindi wa Tuzo hii ya Jamii atapatikana kwa:
 

 
(a)   Mhusika mwenyewe kuwasilisha vielelezo au ushahidi wa mchango wake huo kwa Jamii
 
AU
 
(b)   Kwa jamii kupendekeza jina la mhusika kupitia mitandao ya kijamii
 
AU
 
(c)    Kwa Kamati ya Tuzo ya Jamii kufanya utafiti, kuchambua na kuteua jina moja miongoni mwa yale yaliyopatikana kupitia kipengele (a) na (b)
 

 
Mshindi wa Tuzo ya Jamii 2015 atatangazwa rasmi siku ya Hafla ya Tuzo ya Jamii itakayofanyika tarehe 13 April 2015 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre, Jijini Dar es Salaam
 

 
2. Tuzo ya Jamii-Tuzo ya Heshima
 
Watakaopewa Tuzo ya Jamii-Tuzo ya Heshima ni:
 
(a)  Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na
 

 
(b) Hayati Nelson Mandela –Rais wa Kwanza Mzalendo wa Jamhuri ya Afrika ya Kusini
 
Tuzo hii ya Heshima kwa mwaka huu itatolewa kwa Waasisi hao wawili kutokana na Jitihada na Mchango wao wa kipekee na uliotukuka katika kutetea na Kulinda Maslahi ya Wanyonge
 

 

 
3. Tuzo ya Jamii ya Haki za Binadamu
 
Tuzo hii inatolewa kwa Taasisi au Mtu Binafsi kutokana na Mchango na Jitihada zake katika Kuelimisha, kulinda, kutetea na Kuimarisha Utawala Bora nchini Tanzania
 

 
Vigezo vinavyotumika kwa mwaka huu katika kumpata mshindi wa Tuzo ya Jamii ya Haki za Bianadamu, ni hivi vifuatavyo:
 

 
·         Weredi wa Taasisi au Mtu Binafsi katika kufanya uchunguzi, Utafiti na kutoa taarifa zake kwa uhuru, pasipo upendeleo wowote kwa Serikali, Chama, Kikundi au mtu Binafsi
 
·         Mchango wa Mtu Binafsi au Taasisi katika Kuelimisha Jamii,  kulinda, kutetea na kuhamasisha juu ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini Tanzania.
 

 
·         Mchango wa Mtu Binafsi au Taasisi katika kulinda, kuhifadhi na kuhamasisha juu Amani, utulivu, Usalama wa Raia na Mali zao na Utii wa Sheria kwa ujumla
 

 
  1. Tuzo ya Jamii ya Mwanasiasa Mwenye Mafanikio katika siasa za Tanzania
 

 
Mshindi wa Tuzo hii atatangazwa siku ya hafla ya Tuzo ya Jamii baada ya mwanasiasa husika kupigiwa kura nyingi kupitia mtandao wa Push mobile ambapo mpigaji wa kura anatakiwa aende sehemu ya kuandika ujumbe mfupi wa maneno katika simu yake ya Mkononi na kuandika namba ya Mwanasiasa husika, alafu anatuma namba hiyo kwenda 15522.
 

 
Vigezo vitakavyotumiwa na wapiga kura kupitia namba 15522 ni hivi vifuatavyo:
 

 
  • Uadilifu, Uaminifu, Heshima na Utii kwa Jamii na sheria za nchi kwa Amani ya nchi yetu
 
  • Jitihada binafsi katika kulinda na kutetea Muungano wetu wa Tanganyika na Zanzibar, Umoja wa Kitaifa na Kijamii
 
  • Uzoefu wa Uongozi wa Umma, Taasisi za Kimataifa na Mchango wake kwa Jamii.
 
  • Matarajio, Mipango na nia ya Dhati ya Kuleta Maendeleo na Mafanikio kwa Watanzania
 

 
Orodha ya Wanasiasa wanaowania Tuzo ya Jamii ya Mwanasiasa Kijana na Mtu Mzima Mwenye Mafanikio katika siasa za Tanzania imepatikana baada ya wanajamii kupendekeza mara nyingi jina la Mwanasiasa husika kupitia Mtandao wa Push Mobile na mitandao mingine ya kijamii. Kamati ya Tuzo ya Jamii, baada ya kupitia majina yote yaliyopendekezwa kupitia mbalimbali ikiwemo Push Mobile, imepata orodha ifuatayo:
 

 
WATU WAZIMA
 
JINA LA MWANASIASA
NAMBA YA KUMPIGIA KURA
MHE. MIZENGO PETER PINDA
MM01
MHE. PROF. SOSPETER MWIJARUBI MUHONGO
MM02
MHE. DR. WILBROD PETER SLAA
MM03
MHE. ASHA-ROSE MTENGETI MIGIRO
MM04
MHE. SAMIA HASSAN SULUHU
MM05
MHE. JAMES FRANCIS MBATIA
MM06
MHE. DR. JOHN POMBE MAGUFULI
MM07
MHE. DR. HARRISON GEORGE MWAKYEMBE
MM08
MHE. PROF. IBRAHIM HARUNA LIPUMBA
MM09
MHE. STEPHEN MASATU WASIRA
MM10
MHE. BALOZI LIBERATA MULAMULA
MM11
MHE. BENARD KAMILIUS MEMBE
MM12
MHE. EDWARD NGOYAYI LOWASSA
MM13
 

 
VIJANA
 
JINA LA MWANASIASA
NAMBA YA KUMPIGIA KURA
MHE. JANUARY YUSUPH MAKAMBA
MK01
MHE. ZITTO ZUBERI KABWE
MK02
MHE. MWIGULU LAMECK NCHEMBA
MK03
MHE. HALIMA JAMES MDEE
MK04
MHE. SAADA SALUM MKUYA
MK05
MHE. LAZARO SAMUEL NYALANDU
MK06
MHE. ESTHER AMOS BULAYA
MK07
MHE. UMMY ALLY MWALIMU
MK08
MHE. NAPE MOSES NNAUYE
MK09
MHE .MBONI MHITA
MK10
MHE. DAVID ZACHARIA KAFULILA
MK11
MHE. VICKY PASCHAL KAMATA
MK12
MHE. JOHN JOHN MNYIKA
MK13
 

 
Hatua hii ya upigaji wa kura ni hatua ya mwisho katika mchakato wa kumpata mshindi wa Tuzo ya Jamii ya Mwanasiasa mwenye mafanikio katika siasa za Tanzania (Kijana na Mtu Mzima). Aidha, katika uamuzi wa Mshindi, matokeo ya upigaji wa kura yatachukua asilimia Sabini (70%) na Asilimia Thelathini (30%) zitatumiwa na Majaji ambao ni Kamati ya Tuzo ya Jamii 2015.
 
Zoezi la kumpigia kura Mwanasiasa Mwenye Mafanikio katika siasa za Tanzania limeanza tarehe 10/03/2015 na litaendelea hadi tarehe 13/04/2015.
 

 
MCHAKATO WA JUMLA WA KUWAPATA WASHINDI NA KUWATANGAZA

 
Uendeshaji wa Mchakato wa utoaji wa Tuzo ya Jamii huanzia kwenye Kitengo cha Utafiti, Kumbukumbu na Majadiliano. Kitengo hiki, ndicho chenye jukumu la kufanya tafiti mbalimbali kuhusiana na jambo husika.
 

 
  • Kitengo cha Utafiti, Kumbukumbu na Majadiliano, kinapomaliza kazi yake ya Utafiti, huwasilisha mapendekezo yake kwenye Sekretarieti ya Kampuni ambayo inaundwa na wakuu wote wa vitengo vya kampuni pamoja Wajumbe wengine watatu ambao hufanya idadi yao kufikia saba (7). Kazi ya Sekretarieti ni kupitia taarifa kutoka kitengo cha ya Utafiti, kuichambua na kutoa mapendekezo yake na  kuyawasilisha kwa Uongozi wa Kampuni.
 
  • Taarifa ya Sekretariat huwasilishwa kwa uongozi wa Kampuni kwa ajili ya mapitio, mapendekezo au kwa uongozi kufanya mawasiliano na Vyanzo mbalimbali kabla ya uongozi wa kampuni kuiwasilisha taarifa hiyo kwenye Kamati nzima ya Tuzo ya Jamii
 
  • Kamati ya Tuzo ya Jamii yenye Wajumbe ishirini na sita (26)  ikiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati, hupitia, hujadili na  kuchambua taarifa nzima inayohusiana na kipengele husika cha Tuzo ya Jamii.
 
  • Kamati ya Tuzo ya Jamii baada ya kujiridhisha na uchambuzi iliyoufanya hupitisha, huthibitisha na kutangaza jina moja miongoni mwa yale yaliyohusishwa katika Utafiti husika. Maamuzi ya Kamati ya Tuzo ya Jamii huwa ni ya Mwisho.
 
  • Mhusika aliyeshinda Tuzo ya Jamii katika kipengele husika hupewa taarifa rasmi Kuhusu ushindi wake
 
Imetolewa Machi 18,2015
 
Na Deonatus Julius Malegesi
 
Mwenyekiti
 
Tanzania Awards International Ltd

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA