NACTE YAVIFUNGIA VYUO ZAIDI YA 40 KWA KUKOSA SIFA


Utangulizi
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi ni chombo kilichoanzishwa kwa Sheria ya Bunge Namba 9 ya Mwaka 1997, kwa lengo la kusimamia na kuratibu taaluma zitolewazo na taasisi na vyuo vya elimu ya ufundi nchini, ambavyo siyo vyuo vikuu au vyuo vikuu vishiriki.
Jukumu kubwa la Baraza ni kuendeleza na kuinua ubora wa elimu ya ufundi nchini kwa kusimamia kikamilifu shughuli za uendeshaji mafunzo ili tuzo zitolewazo na vyuo ziwe na ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa.
Notisi
Kwa kutumia Sheria na Kanuni za Baraza [National Council for Technical Education (Registration of Technical Institutions) Regulations, 2001 na National Council for Technical Education (Accreditation and Recognition of Technical Institutions) Regulations, 2001 Baraza linatangaza kwamba linatoa notisi ya siku 30 kwa vyuo/taasisi ziilizokiuka taratibu za Usajili na Ithibati zifuatazo:
a) Vyuo/Taasisi ambazo muda wake wa Usajili wa Awali na Usajili wa Muda umekwisha;
b) Vyuo/Taasisi ambazo zimepitisha muda wa kuanza mchakato wa Ithibati baada ya kupata Usajili Kamili; na
c) Vyuo/Taasisi ambazo muda wake wa Ithibati umekwisha.

Vyuo/taasisi ambazo zinapewa notisi ni kama ilivyoainishwa kwenye Jedwali Na. 1 na Na. 2.







Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA