MATUMIZI MABAYA YA MITANDAO YANASHUSHA MAANA HALISI YA MAWASILIANO

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma
UTUMIAJI mbaya wa huduma za simu na mtandao unaofanywa na baadhi ya Watanzania ndio chanzo cha mambo ya hovyo na yasiyo ya maadili katika huduma ya mawasiliano.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma alipokuwa akifungua warsha ya siku moja kwa wafanyakazi wa mamlaka hiyo katika kuadhimisha Siku ya Mteja inayofikia kilele chake leo.
Alisema matumizi mabaya ya mawasiliano ndiyo yanayofanywa kuwapo kwa taarifa za uzushi na uchochezi, picha na video zisizo na maadili.
“Tatizo hapa si huduma za simu, intaneti, instagram au whatsapp, tatizo ni utumiaji usiofaa unaofanywa na baadhi ya watu. Tunahitaji elimu ya kutosha kwa jamii ya namna ya kutumia vizuri huduma hizi,” alisema.
Alipoulizwa kwa nini Tanzania isiifunge mitandao kama ilivyo China na baadhi ya nchi za kiarabu, Nkoma alisema jambo hilo linawezekana lakini linahitaji fedha nyingi na litarudisha nyuma maendeleo.
Naye Mkurugenzi wa Masuala ya Watumiaji na watoa huduma, Dk Raynold Mfungahema akitoa mada ya majukumu ya TCRA, alisema pamoja na kukua kwa sekta ya mawasiliano, bado huduma zinazotolewa haziridhishi hivyo kuhitaji uwekezaji zaidi.
Aidha, alisema mamlaka yake imekuwa ikipokea malalamiko kadhaa kutoka kwa wateja wa mawasiliano na kubwa ni kuibiwa fedha kwenye simu, kubadilishiwa namba, ujumbe usiohitajika, kutopatikana kwa namba ya huduma kwa wateja, matumizi ya ving’amuzi na madhara ya minara na simu. CHANZO: HABARI LEO

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA