TIKETI ZA TAIFA STARS NA GAMBIA KUANZA KUUZWA JUMAMOSI

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Tiketi kwa ajili ya pambano la Taifa Stars na The Scorpions zitaanza kuuzwa kesho (Juni 9 mwaka huu) kuanzia saa 2 asubuhi kwenye vituo vya Mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Soko Kuu la Kariakoo na Uwanja wa Taifa.
Pia mauzo yatafanyika siku ya mechi kwenye vituo hivyo kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 6 mchana kabla ya kuhamia Uwanja wa Taifa. 
 
 
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani ambavyo ni 36,693 kati ya jumla ya viti 57,558 vilivyopo katika uwanja huo wa kisasa. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ni sh. 5,000.
 
 
Kwa upande wa VIP C watalipa sh. 10,000 wakati VIP B ni sh. 20,000. Kiingilio kwa jukwaa la VIP A ambalo linachukua watazamaji 748 tu ni sh. 30,000 kwa mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni.
 

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA