TBL YATOA SH. MIL 53 KUSAIDIA MRADI WA MAJI CHUO KIKUU CHA ST AUGUSTINE

 Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo (katikati), akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. milioni 53, Naibu  Makamu Mkuu wa Chuo cha St. Augustine (SAUT) Mwanza, Taaluma, Padri Thadeus Mkamwa (kulia) katika hafla iliyofanyika chuoni hapo hivi karibuni. Anayeshuhudia kushoto ni Naibu  Makamu Mkuu wa chuo hicho Utawala na Fedha, Padri Peter Mwanjonde. Msaada huo ni kwa ajili ya mradi wa maji chuoni hapo  pamoja na kilimo cha umwagiliaji.  
  Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo, akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha SAUT, Mwanza, kabla ya kukabidhi mfano wa hundi yenye themani ya shilingi milioni 53 fedha ambazo zimetolewa ili kutekeleza mradi wa maji kwa matumizi ya wanachuo na kilimo cha umwagiliaji. 
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha St. Augustine ( SAUT) Taaluma, Padri Thadeus Mkamwa, (mwenye koti jeusi) akizungumza na wanafunzi na walimu wa chuo hicho muda mfupi kabla ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya shilingi milioni 53 kwa ajili ya mradi wa maji na kilimo cha umwagiliaji. Hundi hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tannzania (TBL), Steve Kilindo (wa pili kutoka kulia) jijini Mwanza hivi karibuni.  Mwenye miwani ni Naibu Makamu Mkuu wa chuo hicho , Utawala na Fedha, Padri Peter Mwanjonde .

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA