WATU WANNE WASHILIKIWA KUHUSIANA NA UJAMBAZI KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI

Na Thomas Dominick,
Musoma
JESHI la Polisi Mkoa wa Mara linawashikilia na kuwahoji watu wanne wanaodaiwa kushirika katika tukio la ujambazi lililotokea June 20, mwaka huu majira ya saa 3:00 usiku Mivaro Campsite iliyopo katika Hifadi ya Taifa ya Serengeti.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Mkoa hapa, Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Absalom Mwakyoma alisema kuwa watuhumiwa hao walipatikana baada ya jeshi hlo kuendesha oparasheni kabambe ambayo ilifanikiwa kuwakamata watu hao.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo ilisema kuwa majambazi wapatao nane walivamia kambi hiyo ya watalii wakiwa bunduki na mapanga, na walipofika karibu na sehemu ya kulia chakula walikutana na Meneja Msaidizi Renatus Robert (42) ambapo walimfyatulia risasi kifuani na kuanguka chini akafariki Dunia.

Baada ya hapo walikwenda kwenye hema namba 12 ambako walikuwepo Mholanzi Erick Paul (58) na kumtaka atoe fedha Uero au dola ambapo aliwaambia watoke ndipo walipompiga risasi ya paja na kumjeruhi kwa mapanga mkono wa kulia na baadaye alifariki dunia kutokana na kuvuja damu nyingi.

Kutokana na milio ya bunduki wananchi wa kijiji cha Ikoma Robanda walielekea kwenye Kambi hilo kwa hamasa kubwa wakiwa na silaha zao kila mmoja aliyoiona inamfaa, wahalifu hao baada ya kusikia sauti zao hawakuendelea na oparasheni yao ya uhalifu wakatoweka kwa kutumia gari walilokuwa wameliegesha porini.

Katika tukio hilo iliwamlazimu wa maliasili na utalii Balozi Khamis Kagasheki na waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Emmanuel Nchimbi kusitisha shughuli za bunge na kufika eneo hilo na kutoa maelekezo yao juu ya kukomesha matukio kama hayo yasijirudie pamoja na kuwataka wamiliki wa Makambi ndani ya Hifadhi hiyo ya Taifa kuwa na walinzi wenye silaha.

Kamanda Mwakyoma alisema kuwa Jeshi hilo linaendelea na ufuatiliaji wa wahalifu hao na kuwaomba wananchi wema kuendelea kushirikiana na Jeshi la polisi kupata taarifa za wahalifu waliobakia ili kwa pamoja wapambane na uhalifu.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA