Redds' miss Mara 2012 kupatikana june 29

Na Shomari Binda
Musoma,

Shindano la kumtafuta Redd's miss Mara 2012 litafanyika June 29 huku waandaji wa shindano hilo kampuni ya Homeland Entertainment$Promotion wakidai asilimia kubwa ya maandalizi ya shindano hilo yamekwisha kukamilika na kinachosubiliwa ni kumpata mrembo wa Mkoa huo atakaye shiriki katika shindano la Redd's miss Tanzania 2012.

Akizungumza na waandishi wa Habari katika kambi ya mazoezi ya warembo wanaotarajiwa kushiriki katika kinyang'anyiro hicho,mkurugenzi wa kampuni ya Homeland Goldon Mkama alisema anawashukuru wale wote ambao wameshiliiki kwa namna moja ama nyingine kutaka kufanikisha shindano la mwaka huu.
Alisema licha ya ugumu wa shughuli za kuandaa shindano hilo la warembo lakini anashukuru mpaka sasa kukamilika kwa asilimia kubwa ya maandalizi yake na kusema kuwa bado kuna nafasi kwa wale wanaohitaji kushiriki kwa namna moja ama nyingine ili kuweza kufanikisha shindano hilo.

Mkama alidai kuwa mpaka sasa warembo 8 wameshafika kambini na kuendelea na mazoezi kwa ajili ya shindano hilo waliopo chini ya msimamizi wa mazoezi hayo miss Lindi na miss Tanzania namba 3 2011Loveness Flavian ambaye kazi yake kubwa ni kuhakikisha warembo watakao shiriki shindano la Redd's miss Mara 2012 wanafanya vizuri.

Muaandaji huyo wa miss Mara 2012 aiwataja warembo ambao wapo kambini mpaka sasa kwa ajili ya kushiriki shindano hilo kuwa ni Rose James,Jacline Mzava,Aisha Bakari,Eugenia Fabian,Jesca Sprian,Justina Thomas,Love Kilasira pamoja na Hellen Mosha
Aidha mkurugenzi huyo wa kampuni ya Homeland aliishukuru kampuni ya African Gold Mine (North Mara) kwa kuendela kuwa mstari wa mbele kwa kutoa udhamini mkubwa kila mwaka katika shindano la kumtafuta mrembo wa miss Mara.

Aliwataja watu wengine waliojitokeza kudahamini shindano hilo kuwa ni chuo cha Musoma Utalii collage,Crdb banki,Coca cola,Maltivilla hotel,Mara security guard,Musoma club,Msendo mini super market pamoja na mtandao wa Shommibindablogspot $ Bindanews.

Aliongeza kuwa katika kusindikiza shindano hilo wasanii mahili wa muziki wa bongo freva Profesa J pamoja na Sharo millionea pamoja na dansa wa twanga pepeta Bokilo Bokilo wanatarajiwa kunogesha shindano.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA