VYUO VIKUU 60 AFRIKA MASHARIKI KUSHIRIKI MAONYESHO JIJINI ARUSHA


Na.Ashura Mohamed-Arusha
Vyuo vikuu 60 zikiwemo taasisi za elimu ya juu na wadau wa vifaa mbalimbali vya elimu kutoka  nchi za Afrika mashariki  wanatarajia kushiriki katika maonyesho  ya huduma na bidhaa zao yatakayofanyika mwezi ujao mjini Arusha.

Mratibu wa maonyesho hayo Peter Oguwi amesema  maonyesho hayo yatakayoanza julai 10 hadi 14 yatafanyika katika viwanja vya nane nane njiro.

Pia  nyatashirikisha vyuo kutoka nje ya afrika mashariki ikiwemo India maonyesho ambayo ameyaelezea kuwa ni ya kipekee na mara ya kwanza kufanyika na yanatarajia kuleta watu zaidi ya 500.

Oguwi amesema lengo la maonyesho hayo ni kutangaza huduma zinazotolewa na vyuo hivyo zikiwemo program mbalimbali ilikuwafanya wananchi wanchi hizo kuthamini vyuo vyao badala ya kukimbilia nchi za nje hivyo maonyesho hayo yana  tarajia kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya elimu ya juu.

Waziri wa elimu na ufundi Shukuru kawambwa anatarajiwa kufungua rasmi maonyesho hayo July 11 mwaka huu Jijini Arusha.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA