MAAFISA MAWASILIANO NA MAHUSIANO WATEMBELEA CHUO CHA SAUT

Maafisa mawasiliano na mahusiano kutoka taasisi mbalimbali na wizara za serikali jana walitembelea chuo kikuu cha mt.Augustino-Mwanza.Maofsa mawasiliano hao ambao wamekuja Mwanza kwenye kikao chao ambapo kinawakutanisha PROs Takribani 50 kutoka sehemu mbalimbali nchini.

 Ziara yao ya kuja SAUT ilikuwa na lengo la kuja kujionea ni kwa jinsi gani chuo kimepiga hatua tangu maafsa hao wahitimu miaka ya hapo nyuma, takribani asilimia 98 ya Maafisa hao wamesomea chuo hiki cha SAUT katika shahada ya kwanza,na shahada ya Uzamivu lakini pia waliambatana na maafsa habari wengine pia ambao wamesomea vyuo tofaut hapa nchini.

Maafsa mawasiliano na uhusiano hao waliweza kukipongeza chuo hiki kwa hatua mbalimbali wanazozichukua katika uboreshaji wa miundombinu, pia na mikakati mizuri kabisa ya kielimu,lakini pia waliweza kukipongeza chuo kwa kutokupandisha ada tangu wao wamalize takribani miaka 8 iliyopita hadi leo ada imebaki kuwa palepale, hivyo chuo kimejidhatiti kuwakomboa kielimu wanafunzi wanaotoka katika familia yenye vipato vya chini 

Makamu mkuu wa chuo Charles Kitima akiwasili eneo la tukio

Maofisa mawasiliano pamoja na wanafunzi wanaosoma mahusiano ya umma katka picha ya pamoja.
                           
Maofsa habari wakienda kuzungushwa na wenyeji wao maeneo mbalimbali ya chuo.

Charles Kitima akiteta jambo pamoja na Msemaji wa jeshi la kujenga Taifa Meja Sipe



Nyanja pamoja na Afsa habari Utumishi wa Umma.(Happy)

Maafsa Uhusiano na mawasiliano wakipokelewa na wahadhiri wa chuo cha SAUT



WANAFUNZI WA SAUT WANAOSOMA SHAHADA YA MAHUSIANO YA UMMA




Clement pamoja David wakionyesha vipaji vyao vya uchekeshaji mbele ya wageni

Moja kati ya Mradi unaoendelea SAUT wa kujenga ukumbi wa mikatano.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA