DEUTSCHE WELLE (DW) KUTUMIA MBINU MPYA YA KUKUFIKISHIA TAARIFA MOJA KWA MOJA KUPITIA WHATSAPP

Mpenzi msikilizaji, msomaji na shabiki wa DW popote pale ulipo, unasemaje kuhusu kupokea habari, picha, vidio na sauti zenye ujumbe wa kukuchangamsha moja kwa moja kwenye simu yako ya mkononi?
Sasa Idhaa ya Kiswahili ya DW inawasiliana nawe moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Sasa Idhaa ya Kiswahili ya DW inawasiliana nawe moja kwa moja kupitia WhatsApp.
DW inakupa huduma hii mpya bila malipo kupitia mtandao wa WhatsApp. Unachohitaji ni simu yako tu yenye huduma ya intaneti na pia WhatsApp. Baada ya hapo fuata hatua zifuatazo kupokea taarifa kutoka kwetu:
1. Hifadhi namba ya WhatsApp ya Idhaa ya Kiswahili ya DW ambayo ni +4915752862185 kwenye simu yako
2. Tuma ujumbe kwa kutumia WhatsApp kwenye namba hiyo ukiwa na neno “Niunge.” Ukipenda, tuambie jina na pia nchi yako.
Baada ya hapo, tutakuweka kwenye orodha ya watu wanaopokea ujumbe kutoka kwetu kila tunapotuma taarifa mpya. Usihofu, hatutakutumia zaidi ya taarifa mbili kwa siku.
Kuwa mmoja wa wanachama wetu wa mwanzo kabisa kwenye jamii ya DW WhatsApp, uwe karibu kabisa na habari mpya na ujumbe wa moja kwa moja kwenye simu yako. DW iko nawe popote ulipo.
Mueleze na rafiki yako kwa kumtumia namba yetu ya simu. Unaweza pia kutufahamisha vile ambavyo ungelipenda kutumia WhatsApp kupokea habari na kututumia ujumbe wa moja kwa moja.
Ikiwa bado wewe hujaanza kutumia WhatsApp na ikiwa simu yako inaweza kutumia huduma hiyo, tafadhali weka sasa kwa simu zinazotumia mifumo ya Android, BlackBerry, Windows, ingia kwenyehttp://www.whatsapp.com/download/.
Usalama wa Taarifa: Namba yako ya simu itatumiwa na DW tu. Usalama wako wakati tunapotumia taarifa zako ni muhimu kwetu. Tunazitumia tu kwa mujibu wa matakwa ya kisheria. Kwa taarifa zaidi juu ya usalama wa taarifa za WhatsApp, tembeleahttp://www.whatsapp.com/legal/.     
mjengwablog.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA