Brazil kumtangaza kocha mpya

Aliyekuwa mkufunzi wa timu ya soka ya Brazil Luiz Felipe Scolari
Brazil inatarajiwa kumtangaza mkufunzi wake mpya katika mkutano na wanahabari siku ya jumanne kufuatia kujiuzulu kwa kocha wa timu hiyo Luiz Felipe Scolari.

Scolari mwenye umri wa miaka 65 aliiongoza Brazil katika semi fainali za kombe la dunia ambapo timu hiyo ilipata kichapo kibaya cha mabao masaba kwa moja dhidi ya mabingwa wa kombe la Dunia Ujerumani.

Aliyekuwa kocha wa timu hiyo ambaye aliiongoza timu hiyo kati ya mwaka 2006 na 2011 huenda akarejea na kuchukua kazi hiyo.

Wengine wanaopgiwa debe kuchukua kazi hiyo ni mkufunzi wa kilabu ya Corinthians Tite,Mkufunzi wa kilabu ya Sau Paulo Muriciy Ramalho na Vanderlei Luxembourg ambaye aliwahi kuifunza timu hiyo kutoka mwaka 1998 hadi mwaka 2000.

Chanzo BBC

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA