CHANGAMKIA FURSA YA MAFUNZO BURE, JINSI YA KUTUMIA FACEBOOK KIBIASHARA KWA WAJASILIAMALI



Katika dunia ya leo, kama wewe ni mfanyabiashara basi hauwezi epuka ushawishi wa mitandao jamii. Ingawa wengi wetu tumekuwa tukiitumia mitandao jamii kwa ajili ya mawasiliano pekee, ila kuna mengi yanaweza kufanyika na kusaidia kukuza ufannisi wa biashara yako.
Kwa kulitambua hilo, Dudumizi Technologies LTD inakuletea mafunzo juu ya njia na namna sahihi za kutumia Facebook kukuza na kuboresha Biashara.
Mafunzo haya yatakuwa ya wiki mbili, bila kukuchosha (tukitambua muda ni kitu muhimu kwa mjasiriamali), tutakutumia dondoo (kwa email fupi) iliyojikita moja kwa moja kwenye utendaji. Hivyo, kila siku utapokea email moja inayokufundisha jinsi ya kutekeleza hatua husika. Mwisho wa siku, utakuwa umejijngea uwezo mkubwa wa kutumia Facebook kwa ajili ya biashara yako.
 Pia, washiriki wote watapata nafasi ya kuuliza maswali kwa email kwenda kwa wataalamu wetu kwa muda wote wa mafunzo bila gharama yoyote. Pia washiriki watajumuishwa kwenye muendelezo wa mafunzo ya matumizi mbalimbali IT kwenye biashara kwa Video kwa siku za usoni.

Walengwa: Wamiliki wa biashara wadogo na wa kati
Gharama: Bure, unachotakiwa ni kujiunga tu na fomu ya mlisho wa email chini
Muda wa mafunzo:  July 21 - Agosti 5
Muda wa mwisho kujiunga: July 20
Idadi ya Washiriki: 100
Lugha: Kiswahili
Muandaaji: Dudumizi Technologies LTD  

CHANZO:DUDUMIZI WEB

Fomu ya Kujiunga bofya Hapa

 

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA