NYALANDU AJITOSA RASMI MBIO ZA URAIS KUPITIA CCM 2015

WAZIRI wa maliasili na utalii na mbunge wa jimbo la Singida kaskazini(CCM) ,Lazaro Samwel Nyalandu, ambaye ametangaza rasmi kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.  

Na Gasper Andrew, Mwananchi
 

WAZIRI wa maliasili na utalii na mbunge wa jimbo la Singida kaskazini(CCM) ,Lazaro Samwel Nyalandu,ametangaza rasmi nia ya kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.
Nyalandu ametangaza nia hiyo leo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Ilongero Jimbo la Singida kaskazini.
Alisema baada ya kutafakari kwa muda mrefu na kujikagua kwa kina,ameona anao uwezo wa kutosha wa kuweza kupokea kijiti kutoka kwa rais anayemaliza muda wake mwakani kwa mujibu wa katiba.
“Kujikagua huko ni pamoja na kutafakari jinsi alivyoweza kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM katika vipindi vitatu (miaka 15) akiwa mbunge wa jimbo la Singida kaskazini.Katika kipindi hicho cha ubunge,nimeweza kutumia zaidi ya shilingi bilioni mbili katika kufanikisha kuchangia miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali zikiwemo za afya,maji na barabara”,alisema Nyalandu.
Alisema wakati ukifika,Watanzania kutoka sehemu mbalimbali za nchi wakiongozwa na wakazi wengi wa kutoka jimbo la Singida kaskazini,kwenda Dodoma kuchukua fomu za kuwania urais.
“Watanzania waliokwisha onyesha nia ya kuwania urais mwakani,nawaomba sote tuonyeshe kazi tulizozifanya katika kuwahudumia Watanzania,ili waweze kutupima vizuri waweze kujijengea mazingira mazuri ya kuchangua rais atakayewafaa kwa kuwaletea maendeleo endelevu”,alisema.
Nyalandu alisema kuwa anakishukuru Chama Cha Mapinduzi,kwa maandalizi yake mazuri ya kuhakikisha chama kinapata mwanaCCM safi,mwadilifu na mchapa kazi atakayepeperusha bendera ya chama katika kinyang’anyiro cha kuwania urais mwakani.

CHANZO:mwananchi.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA