BINTI AJIRUSHA BAHARINI

Mwanadada mmoja amejirusha baharini katika kivuko cha ferry mapema leo adhuhuri wakati akiwa ameabiri ferry ya MV Harambee kutoka upande wa Mombasa Kisiwani kuelekea Likoni.

Msichana huyo mwenye umri kati ya miaka 20 na 25 amejirusha kutoka eneo la juu ya ferry wakati fery ikiwa katikakati ya bahari ikielekea ufuoni.

Wapiga mbizi wa shirika la Kenya ferry wamejaribu kuokoa maisha yake baada maji kumzidi kutokana na mawimbi makali na akafanyiwa huduma ya kwanza na hatimaye kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Likoni. Kwa sasa anapokea matibabu katika hospitali moja mjini Mombasa.

Kulingana na afisa wa uhusiano mwema wa shirika la Kenya Ferry Harun Mutiso amesema kwamba maafisa wa polisi wanachunguza kilichopelekea msichana huyo kutaka kutoa uhai wake.

Hata hivyo kulingana na walioshuhudia ni kwamba wanadada huyo alionekana mtulivu na hakuna aliyetarajia kwamba anaweza jirusha kutoka eneo la juu ya Ferry hadi ndani ya bahari.

Haya yanajiri siku moja baada ya mwanadada mmoja kutoka mtaa wa wa mbuzi huko Likoni kumtumia rafiki yake wa kiumeujumbe mfupi kutumia simu ya rununu kwamba atajinyonga kutokana na hali ya maisha kuzidi kuwa ngumu kwake.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA