MAJAMBAZI WA DRC WAUA POLISI WA TANZANIA

ASKARI mmoja wa Tanzania amepoteza maisha baada ya kutokea mapigano katikati ya Ziwa Tanganyika kati ya majambazi yenye silaha toka nchi jirani na askari wa Tanzania wakiwamo polisi na wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Taarifa zilizoripotiwa katika mtandao wa JamiiForums.com na kuthibitishwa na polisi zimeeleza kwamba askari wa Tanzania akiwamo Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Kigoma Mohamed Kilonzo, walikwenda kumuokoa Mtanzania aliyetekwa na majambazi hayo na kutokea mapigano hayo.

Katika tukio hilo majambazi wote sita waliuwawa na askari mmoja wa Tanzania alifariki kutokana na majeraha makubwa wakati wengine sita wakiwamo askari wa JWTZ walijeruhiwa baadhi yao vibaya sana.
Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma Frassa Kashai, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuahidi kulitolea taarifa tukio hilo baadaye, kwa kuwa wakati huo walikuwa wakishughulikia suala hilo ikiwa ni pamoja na kuwahudumia majeruhi na kufuatilia usalama wa eneo hilo.


Taarifa katika mtandao wa JamiiForums.com zilizotumwa na mwanachama wa mtandaoa huo mwenye jina la KAUMZA zilieleza;
“Leo mchana kumetokea mapigano makali kati ya askari wa jeshi la polisi na JWTZ kwa upande mmoja na majambazi kutoka Congo (DRC). Katika mapigano hayo Oc-cid wa Kigoma bwana Mohamed Kilonzo amepigwa risasi kifuani pamoja na askari polisi mwingine amepigwa risasi ya shingo. Kwa upande wa JWTZ, askari mmoja kavunjwa miguu, mwingine risasi imeingia kiunoni na mwingine kapigwa mkononi.
“Hadi ninapoleta taarifa hii, majeruhi wapo theatre takribani masaa manne sasa na madaktari wanaendelea kufanya jitihada za kuwasaidia. Na kwa upande wa adui, habari zilizopo ni kuwa wote wameuawa. Chanzo cha tukio hili ni kuwa majambazi hao kutoka Congo kumteka raia wa Tanzania na askari wetu kutaka kumuokoa. Tuombe Mungu awaponye”
Taarifa zaidi tutaendelea kuwaletea huku ukifuatilia: Mapigano katika Ziwa Tanganyika

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA