UFUNGUZI WA SAUT BUSINESS INCUBATION CENTRE

Kesho tarehe 31/05/2012 kuanzia saa 8:00 Mchana- 11:30 katika ukumbi wa M12 katika chuo kikuu cha Mt.Augustino kutakuwa na uzinduzi rasmi wa kituo cha ujasiliamali kitakachojulikana kwa jina la BUSINESS INCUBATION CENTRE (B.I.C).

Centre hii ni mahususi kabisa katika kutoa elimu ya ujasiliamali kwa wanafunzi wote wa SAUT ambao watakuwa mwaka wa mwisho wa masomo yaani mwaka wa 3 na 4,baada ya kumaliza mitihani yao ya mwisho wa semister watapata fursa ya kuweza kupata mavunzo ya ujasiliamali kwa muda wa miezi 3 BURE kabisa,ambapo chuo kimejitolea kutoa majengo yake,kuleta walimu kutoka sehemu tofauti tofauti hapa nchini na nje ya nchi.

Dhumuni la kuanzisha Centre hii ni kuweza kuwasaidia hususan wanafunzi wa SAUT na jamii kwa ujumla njia tofauti tofauti za kuweza kupata fursa za kujiajiri wao wenyewe kwa kuanzisha makampuni yao na pia kuweza kuwapatia mwanga juu ya jinsi gani wanaweza kutumia malighafi zilizopo nchini na kuweza kumiliki njia kuu za uchumi kwa maendeleo ya jamii na pia kwa nchi kwa ujumla badala ya kuwategemea wawekezaji waweze kushikilia njia hizo wakati wanazuoni wapotele hapa nchini huku wakiangaika kwa kutembea na Bahasha mkononi wakiomba ajira katika makampuni na ofsi mbalimbali hapa nchini. 

Center hii itakuwa endelevu,hivyo basi wanafunzi wote  wa kutoka kozi zote za hapa SAUT wanaomaliza masomo yao wanaombwa kuchangamkia nafasi hii ya kipekee kabisa kuweza kutokea hapa SAUT na ndani ya vyuo vya hapa nchini,pia wajasiriamali wa hapa nchini waliofanikiwa watapata fursa ya kuweza kutoa ushuhuda wao ni kwa jinsi gani wameweza kufikia malengo yao waliokuwa wamejiwekea na hatua ambazo wamezitumia mpaka hapa walipofikia,nia ni kuweza kuleta uhalisia halisi kwa wanafunzi hao wakati wa mafunzo. mafunzo haya yatakuwa yamejikita zaidi katika vitendo.

kwa wale wanafunzi watakaoweza kufanya vizuri kwa kuja na michanganuo ya kibiashara (Business plan) zao zitakazokuwa zimeandaliwa vizuri, basi baada ya masomo chuo kitaweza kuwawezesha kwa kuwapatia fedha kwa ajili ya kuanzisha biashara zao.

Vyombo vya habari,makampuni ya kibiashara mnakaribishwa sana katika uzinduzi huu.
             Mnakaribishwa nyote. 



Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA