WAUGUZI WA HOSPITALI YA MKOA WA MARA WAGOMA

Wauguzi katika hospitali ya Mkoa wa Mara wameweka mgomo wa kuingia wodini na kutoa huduma mbalimbali katika hospitali hiyo wakishinikiza uongozi wa hospitali hiyo kuwalipa madai yao mbalimbali ambayo wanadai na kusema kuwa hawatafanya kazi mpaka hapo watakapo tekelezewa.

Mgomo huo wa wauguzi umeanza leo asubuhi baada ya wauguzi hao kufika kazini na kushindwa kufanya kazi huku wakisema kuwa wamenyanyaswa vya kutosha na wanachotaka nikulipwa madai yao ndipo huduma kutoka kwao ziweze kuendelea katika hospitali hiyo.

Kutokana na mgomo huo kumesababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa wa wodini na wale wa nje baada ya kukosa huduma mbalimbali huku wengine wakitupia lawama kwa uongozi wa hospitali hiyo kwa kushindwa kukaa na wauguzi hao na kufika muafaka ili waendelelee kupata huduma kama kawaida.

Mmoja wa wauguzi wa hospitali hiyo Antunia Machibula alisema kuwa kutokana na kushindwa kuthaminiwa kutokana na kupuuzwa kwa malipo yao na shughuli wanazozifanya wameamua kufanya hivyo ili kushinikiza kulipwa malipo yao wanayoyadai na kusema kuwa malipo wanayodai tayari yalishatolewa kutoka katika ofisi za ngazi ya juu zinazohusika.

Amesema kuwa baada ya kutokea mgomo wa madaktari miezi michache iliyopita ofisi ya Waziri Mkuu ilifanya malipo yote yanayohusiana na madaktari na waauguzi lakini cha kushangaza wao wameshindwa kulipwa huku wengine wakilipwa kiwango ambacho akistahili katika malipo yaliyokuwa yamekokotolewa.

"Kwa mfano yule muuguzi ambaye anatakiwa kulipwa malipo ya ziada ya shilingi elfu kumi analipwa shilingi elfu tano na yule anaetakiwa kulipwa shilingi shilingi elfu ishilini analipwa elfu kumi sasa hii sisis tunaona ni manyanyaso kwetu na tunaomba jamii ituelewe hivyo maana tumechoka kunyanyaswa",alisema Machibula.

Kwa upande wake muuguzi Juma Warioba alisema kuwa ofisi ya Waziri Mkuu ilitoa kiasi cha shilingi milioni 40 kutokana na madai mbalimbali yanayowahusu lakini wanashangazwa na kutokulipwa kama inavyostahili licha ya kukaa vikao mbalimbali kuzungumzia suala hilo na kilichobaki ni kutokufanya kazi mpaka pale madai yao yatakaposikilizwa.

Baada ya maelezo hayo ya wauguzi wa hospitali hiyo ya Mkoa wa Mara kueleza madai yao BINDA NEWS lilifika katika ma wodi ya hospitali hiyo na kukuta wagonjwa wakiwa pekee yao huku kukiwa hakuna huduma mbalimbali zinazoendela za kimatibabu na kulalamikia kile ambacho kilikuwa kikiendelea katika hospitali hiyo.

Mmoja wa wagonjwa waliokuwa wamelazwa katika wodi namba saba aliyejitambulisha kwa jina la Musa Mikidadi alisema tangu asubuhi ajapata huduma yeyote licha ya kutakiwa kupata huduma kutwa mara tatu na kudai kuwa kuna mmoja wa wagonjwa jamaa zake walilazimika kumtoa nje ya wodini na kwenda kutibiwa katika vituo binafsi.

Sakata lingine likatokea katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali hiyo baada ya muhudumu wa chumba hicho nae kuweka mgomo wa kutoa wala kupokea maiti katika chumba hicho kwa kuwa kufanya hivyo ni sawa na kuwasaliti wenzake kwa kuwa wote wapo katika mgomo wa madai ya kimaslahi.

Muhudumu huyo aliyejitambulisha kwa jina la Masatu Masatu alisema kuwa hataweza kufanya kazi yeyote mpaka hapo utakapapatikana muafaka ambao wanaudai kutoka kwa viongozi licha ya kuwepo kwa watu waliokuwa wakihitaji huduma ya kuwatoa ndugu zao katika chumba hicho cha kuhifadhia maiti.

Kutokana na sakata hilo kulipikea katibu tawala wa wilaya ya Musoma ambaye ni kaimu mkuu wa Wilaya ya Musoma kufika katika hospitali hiyo akiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya Debora Makinga ili kuzungumza na wauguzi hao lakini hadi majira ya saa 8;40 alasiri kulikuwa hakujapatikana muafaka wowote kati ya wauguzi na viongozi hao.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA