ARGENTINA YATINGA FAINALI BAADA YA KUITOA UHOLANZI KWA PENATI 4-2
NDOTO za Argentina kutwaa kombe
la dunia mwaka huu katika ardhi ya majirani zao Brazil zimeendelea
kuwepo baada ya kuipiga Uholanzi kwa mikwaju ya penati 4-2.
Mechi hii kali ya nusu fainali ya pili imekwenda mpaka dakika 120, lakini matokeo yalisimama 0-0.
Mlinda mlango wa Agrgentina, Sergio Romero alikuwa shujaa baada ya kuokoa penati mbili za Ron Vlaar na Wesley Sneijder.
Waamerika kusini hao walifunga
penati zao zote nne na sasa watacheza fainali dhidi ya Ujerumani, siku
ya jumapili katika dimba la Maracana.
Lionel Messi alibanwa na wachezaji wa Uholanzi na kushindwa kuleta madhara.
Naye Robin Van Persie alifichwa kabisa na alitolewa katika dakika za nyongeza.
Gonzalo Higuain alipoteza nafasi muhimu ya kufunga katika dakika za kawaida.

Kichwa kwa kichwa: Ezequiel Garay na Robin van Persie waligongana


Comments
Post a Comment