BANGI RUKSA KUUZWA WASHINGTON

Uuzaji wa bangi kama ulevi wa starehe utaanza kuuzwa rasmi hii leo katika jimbo la Marekani la Washington. Hili ni jimbo la pili nchini humo kuhalalisha bangi kwa matumizi ya burudani, baada ya jimbo la Colorado kufanya hivyo. Mapato ya kodi kutokana na uuzaji wa bangi katika jimbo la Colorado yamefikia dola milioni kadhaa sasa. Mchakato huo utadhibitiwa kwa makini katika jimbo la Washington.

Maduka ishirini na tano tu ndio yamepata leseni ya kuuza mpaka sasa, ingawa maafisa wanasema idadi hiyo huenda ikaongezeka na kufikia maduka takriban mia moja. 

Majimbo mengine 23 nchini Marekani tayari yanaruhusu uuzaji na ununuaji wa bangi lakini kwa sababu za kitabibu.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA