RAY C AFUNGUKA NA KUMJIBU TID MNYAMA BAADA YA KUMTUKUNA INSTAGRAM.
Wiki iliyopita kulitokea mgogoro wa kupishana kauli baana ya mwanamuziki wawili Ray C Na TID, jambo lililopelekea mtandao wa instagram kuwa uwanja wa mapambano kati ya fans wa TID na Ray C baada ya TID kuandika maandishi yasiyo faa kuandikwa tena mahali hapa.
Ugomvi huo unahusisha zaidi swala la madawa ya kulevya ambapo kumekuwa na tetesi kuwa TID amekuwa akitumia hivyo Ray C alikuwa anampa kama ushauri hapo ndipo zogo lilipotokea.
LEO kupitia mtandao wa kijamii wa instagram Ray C kaamua kufunguka kuhusu kauli hiyo ya mnyama TID.
" rayc1982 Hi everyone!!!Asanteni kwa maombi yenu!mama anaendelea vizuri Mungu ni Mwema............(na kuhusu @tidmnyama -Nimeona post yako,Asante kwa matusi yako ila sikuwa na nia mbaya tofauti na ulivyofikiria anyway Nakuombea kwa Mungu akuepushe na majanga ya dunia!ubarikiwe sana babaa."
Comments
Post a Comment