MAMIA WAJITOKEZA KUUAGA MWILI WA KIONGOZI WA CHADEMA-ARUSHA
Jeneza
lenye mwili wa marehemu Msafiri Jonathan Mbwambo (38) likishushwa
kwenye gari kwa maandalizi ya wananchi kutoa heshima zao za mwisho
katika viwanja vya Ngusero, Usa-River jana. Shughuli hiyo ilihudhuriwa
na viongozi mbalimbali wa dini, viongozi wa chama, RPC wa Mkoa wa
Arusha, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, OCD wa Arumeru na wananchi wengine.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye (katikati) akifuatilia
hotuba za wasemaji wa makundi ya jamii yaliyowakilishwa. Kutoka kushoto
anaonekana kwa mbali Mh Vicent Nyerere (Musoma), Mh Joshua Nassari
(Arumeru Mashariki), Mh Godbless Lema, Mh Cecilia (Viti Maalumu),
Kamanda Andengenye, na OCD John wa Arumeru
Kamanda
Andengenye akisalimia wananchi. Baadae aliahidi kuwa Jeshi lake
litatoa zawadi ya shilingi milioni 10 kwa mtu atakaesaidia kupatikana
kwa waliohusika na mauaji hayo na kwamba Polisi watahakikisha
wanawasaka wahalifu hao kwa udi na uvumba hadi wapatikane.
Mbunge
wa Arumeru Mashariki, Mh Joshua Nassari (CHADEMA) akizungumza kwa
hisia kuhusiana na mauaji yanayowaandama viongozi wa chama chake
Mbunge
wa Musoma, Mh Vicent Nyerere akitoa heshima za mwisho. Mh Vicent ndie
alieteuliwa kuwakilisha chama chake katika maziko yanayofanyika leo
kijijini kwa Marehemu, Same-Kilimanjaro
Kuna walioshindwa kujizuia na kuishia kuangua kilio. Simanzi kubwa
Msiba ulikuwa mchungu kwa kada nyingine za siasa pia, na si CHADEMA pekee
Kuna waliopandisha mori kama huyu mama. Hapa anaondolewa eneo la viwanja hivyo
Aliekuwa
Mbunge wa Arusha Mjini, Mh Godbless Lema akielekea kutoa heshima za
mwisho akiwa ameambatana na mtoto wake. Nyuma yake ni Mbunge mpya Viti
Maalumu, Mh Cecilia aliechukua nafasi ya marehemu Regia Mtema aliekufa
kwa ajali ya gari mapema mwaka huu.
Watoto walioachwa na marehemu
Mke wa marehemu akifarijiwa na majirani zake
Baadhi
ya viongozi wa Baraza la Vijana CHADEMA Mkoa wa Arusha wakijadiliana
jambo ukiwa unasubiriwa msafara wa kusafirisha mwili wa marehemu kwenda
Same uanze kuondoka
SOURCE www.freebongo.blogspot.com
Comments
Post a Comment